Tuesday, March 12, 2019
Friday, May 18, 2018
*JE NI HALALI KI-BIBLIA MWANAMKE KUHUBIRI KANISANI*
*AU*
*KUWA MCHUNGAJI ❓*
( Sehemu ya kwanza )
<><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><>
Mistari muhimu ya kukumbuka:-
*1 WAKORINTHO 14:34-36:-*
*34 Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.*
*35 Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.*
36 Au je! Neno la Mungu lilitoka kwenu? Au kuwafikia ninyi peke yenu?
*1 TIMOTHEO 2:11-12:-*
11 Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.
*12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.*
πππππππππ
HII NI MADA YENYE UBISHI MKUBWA miongoni mwa vichwa vya watu wengi . Na maandiko hayo kwa kueleweka isivyo sahihi hutumiwa na baadhi ya watu wengi kujaribu kujenga hoja zao za kupinga kwamba mwanamke hana haki yoyote ya kuwa Mchungaji wala kusimama madhabahuni kuwahubiria watu kanisani.
Jambo hili limeleta mzozano mkubwa na mpasuko ndani ya makanisa mengi ya Mungu, kuhusu uhalali wa mwanamke kuhubiri madhabahuni na kuwa Mchungaji. Kuna mawazo ya positive na Negative, kuna wengine wanaona ni sahihi na kuna wengine kwao siyo sahihi kabisa .
Sasa basi ukweli na usahihi wa maandiko hayo ni upi basi? Je, ni sahihi kwamba mwanamke hatakiwi kuhubiri madhabahuni kanisani au kuwa Mchungaji ? Tatizo ni kwamba Maandiko hayo hayaeleweki vizuri kwa kwa wakristo wengi na hata baadhi ya wachungaji na Maaskofu, wanalifafanua hilo Andiko kwa maana potofu kabisa .
*NB:-*
Kuitwa Mtume, Nabii Askofu au Mchungaji n.k. Siyo kigezo kikubwa cha kwamba wewe unaielewa sana Biblia kwa usahihi wake. La asha ! Ndiomaana wako hata wachungaji wengine tena wengi tu ambao huyatafsiri maandiko isivyo na kuyapotosha kwa tamaa zao wenyewe.
MWALIMU MKUU WA BIBLIA NI ROHO MTAKATIFU; yeye ndiye aliyeyaleta maandiko hayo kwetu. Na hatuwezi sisi kuamua kuyatafsiri maandiko hayo vyovyote tu kama apendavyo mtu fulani kutafsiri. La Asha
*[ 2 PETRO 1:19-20 ]*.
Bali katika kanuni za kuyatafsiri maandiko, tunahitaji sana maongozi ya msaada wa Roho Mtakatifu mwenyewe katika kuyasoma na kuyaelewa maandiko vizuri na kuyatafsiri kwa usahihi wake. Neno la Biblia. Tunaweza kulifaham kwa kufunuliwa na Roho Mtakatifu pekee yake. Ndiomaana Yesu alisema *uliwaficha wenye hekima na Akili (Wasomi), ukawafunulia watoto wachanga (Watu wasio na elimu)*. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza mbele zako [ MATHAYO 11:25-26]. *"Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho Mtakatifu*. Maana Roho huchunguza yote hata mafumbo ya Mungu. Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, *bali Roho atokaye kwa Mungu makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu "*.
[1 WAKORINTHO 2:10-15].
Si hilo tu. Nikodemo alikuwa ni mwalimu mkuu wa chuo cha Torati. Na watu walimwamini sana katika Taifa la Israeli. Lakini Nikodemo alipoambiwa na Yesu maneno mepesi tu ya Mungu , na usomi wake wote, alishindwa kuyaelewa maana yake nini !! Sasa Yesu ambaye hakupita chuo chochote cha Theolojia, ikambidi amfundishe Nikodemo, mwalimu mkuu wa chuo cha Theolojia ya Torati.
[ YOHANA 3:1- 10 ]
Sisemi wala kupinga kwamba kusoma chuo cha Biblia ni kosa au ni vibaya, au ni dhambi. Hapana. Ni nini maana ya kuanza kukwambia hayo. Maana yangu ni hii kwamba :- Ondoa dhana potofu ukafikili kila mtu anayeitwa Mchungaji, Askofu au Mwanatheolojia fulani msomi anaielewa sana Biblia ki-maana. Ukiwa na mawazo hayo tu, utapotezwa na kudanganyika sana Mpendwa . Na Mungu huwa hatendi kazi kwa misingi hiyo. Mchungaji /Ev/ Mwanatheolojia huyo *Anaweza kuielewa Biblia kwa namna fulani tu ya akili hivi , lakini asiweze kabisa kuielewa Biblia kwa jinsi ya rohoni zaidi kwa ufunuo wa Roho Mtakatifu*. Na maana ya kweli ya maneno ya Biblia hutumbalikana kwa jinsi ya rohoni zaidi na sio kwa jinsi ya mwilini.
[ WAGALATIA 1:11-12 ; WAEFESO 1:17-19].
Hivyo ni vema zaidi tusiweke vipimo vyetu vya usomi kama kigezo cha kuitafsiri Biblia; bali tumuhitaji sana Roho wa Mungu ndio atuongoze katika kulitafsiri Neno lake Mungu.
*Je, ni halali Mwanamke kuhubiri au kuwa Mchungaji?*
Jibu :- Ni ndiyo kwa herufi kubwa.
Tutajifunza somo hili kwa kuligawa katika vipengele vinne. Ambavyo ni :-
*(1) HOJA POTOFU KUHUSU MWANAMKE KUTOKUWA MCHUNGAJI / MUHUBIRI.*
*(2) UHALALI WA MWANAMKE KUHUBIRI / KUFUNDISHA KANISANI*.
*(3) UHALALI WA MWANAMKE KUWA MCHUNGAJI*
*(4) UFAFANUZI WA ANDIKO LA 1 WAKORINTHO 14:34-35 NA 1 TIMOHEO 2:12*.
KIPENGELE NO:1
*HOJA POTOFU KUHUSU MWANAMKE KUTOKUWA MCHUNGAJI/ MUHUBILI*.
Ukiwasikia watu wengi wanaopinga mwanamke kuhubiri au kuwa Mchungaji. Mbali na kutumia Andiko la 1 Wakorintho 14:34-35 na 1 Timoheo 2:12-15 katika ufafanuzi wao .
Pia watajenga hoja yao nyingine ni kwamba *MWANAMKE NI KIUMBE DHAIFU* na hivyo wataeleza mengi tu katika kufafanua hoja yao hii.
Lakini mbele za Mungu, hoja ya mwanamke kutokuhubiri au kuwa Mchungaji kwa sababu eti ni kiumbe dhaifu. Hoja kama hii haikubaliki na wala haina maana yoyote. Kwa sababu Biblia inasema kwamba *Hao hao watu walio dhaifu machoni petu ndio Mungu anayewachagua kuwa watumishi wake*. Neno la Mungu linasema katika
*1WAKORINTHO 1: 26-29:-" Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; TENA MUNGU ALIVICHAGUA VITU VINYONGE VYA DUNIA NA VILIVYODHARAULIWA (WANAWAKE), naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu."*
Kwa maana hiyo ni muhimu kuzidi kuelewa na kufaham vizuri kwamba siku zote Mungu huwa hamchagui mtu yoyote kuwa mtumishi wake katika ngazi yoyote ya utumishi wa kihuduma kwa sababu tu ya kigezo cha jinsia yake kwamba ni kike au kiume. Hapana. Mungu hachagui mtu yoyote kwa kigezo cha sifa, umri, cheo au jinsia yake. Mungu huwa hatumikiwi wala kutenda kazi kwa misingi hiyo. Biblia inatuambia katika
*1 SAMWELI 16:7-10*:-
*7. Lakini BWANA akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. BWANA HAANGALII KAMA BINADAMU AANGALIAVYO; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali BWANA huutazama moyo.*
8. Ndipo Yese akamwita Abinadabu, akampitisha mbele ya Samweli. Naye *akasema, BWANA hakumchagua huyu*.
9. Ndipo Yese akampitisha Shama. *Naye akasema, wala BWANA hakumchagua huyu*.
10. Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli. *Samweli akamwambia Yese, BWANA hakuwachagua hawa*.
*WAFILIPI 3:3-4:-"Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, WALA HATUUTUMAINI MWILI. Walakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu ye yote akijiona kuwa anayo sababu ya kuutumainia mwili, mimi zaidi."*
Kwa sababu hiyo. Mungu katika mpango wake anaweza kumchagua mtu yoyote yule bila kujali sifa yake, umri wake au jinsia yake kwamba ni *mwanamke* au mwanaume , Mungu anaweza kumchagua awe mtumishi wake katika ngazi yoyote ya utumishi na tena akamtumia kwa viwango visivyo vya kawaida. Kwa hiyo sisi wanadamu hatupaswi kuamua kumpangia Mungu kwamba mwanamke hawezi kuwa Mchungaji au muhubiri. Kivipi !? *TUSILETE MFUMO-DUME NDANI YA KANISA LA MUNGU*. Hilo ni chaguo la Mungu sio la kwako wewe mwanadamu. Na kwa maana hiyo Mungu akiamua kumchagua mwanamke kuwa Mchungaji, Askofu, Mwinjilisti, mtume, Nabii n. k. Atakuwa hivyo Mchungaji, mtume, Nabii na kadhalika. Biblia inasema katika
*WARUMI 9:11-16*:-"
(kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, *ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye)*, aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo. Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia. Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha!
Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. *Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu."*
*WAEBRANIA 5:4:-" Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ILA YEYE AITWAYE NA MUNGU*, kama vile Haruni ".
Na kwa maana hiyo. Ngazi yoyote ya utumishi katika huduma mtu huwekwa na Mungu . Mungu akiamua kumwita mwanamke awe mchungaji, atakuwa ni Mchungaji tu na Mungu atajidhihirisha kwake kwa kumthibitisha kwamba yeye ndiye aliyemuita. *Wako wachungaji wanawake na wahubiri duniani ambao Mungu anawatumia kwa viwango vya juu sana katika huduma zao*. Hatuwezi kukanusha na kupinga utumishi wao kwa sababu tu ya kijinsia. *Yesu alisema kama hamniamini mimi, ziamini zile kazi , kwa kuwa kazi zenyewe zanishuhudia ya kwamba Baba Mungu amenituma*.
[ YOHANA 5:36; YOHANA 10:25, 36-38; YOHANA 14:10-12].
*HOJA YAO YA PILI.*
*Watasema hata maandiko yanamtaja kwamba mwanaume ndiye anayepaswa kuwa Mchungaji (Askofu). Uaskofu ni ngazi ya juu ya madaraka ya kichungaji*.
Na watatumia Andiko lao hili lifuatalo katika
*1 TIMOHEO 3:1-12:-*
1-7. Ni neno la kuaminiwa; *mtu akitaka kazi ya askofu*, atamani kazi njema. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, *MUME(MWANAUME) wa mke mmoja*, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha; mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)
Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.
Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.
8-12. *Vivyo hivyo mashemasi* na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana, si watu wanaotamani fedha ya aibu; wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia. Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; si wasingiziaji; watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.
*Mashemasi na wawe WAUME wa mke mmoja*, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao. Kwa maana watendao vema kazi ya shemasi hujipatia daraja nzuri, na ujasiri mwingi katika imani iliyo katika Kristo Yesu. "
Ni muhimu kuelewa vizuri Andiko hilo kwa kusema *mwanaume hapo ndiwe Askofu*. Haimanishi kwamba basi limemkataza Mwanamke asiwe mchungaji au Askofu. Hapana. Kwa sababu ukitazama mukadha mzima wa maelezo yote ya Andiko nzima, yameendelea kusema pia *" MASHEMASI NA WAWE WAUME wa mke mmoja "*. Sasa Je, kwa kusema hivyo tuseme Paulo Mtume hapo hakuwaruhusu pia wanawake wasiwe washemasi kwa sababu tu amewataja wanaume? Jibu ni hapana.
Tunaona pia walikuwepo *MASHEMASI WANAWAKE* ambao pia Paulo mtume aliwachagua katika kanisa. Ukisoma katika *WARUMI 16:1*, Biblia inasema:- *" Namkabidhi kwenu Fibi, Ndugu yetu, aliye muhudumu wa kanisa lililoko Kenkrea"*. Mstari huo katika Biblia ya kingereza ya *New International Version*, unasomeka hivi, *Romans 16:1:-" I commend to you our Sister Phoebe, a Servant (deaconess) of the church in Cenchrea"*.
Kwa hiyo tunaona hapo juu ya Shemasi Mwanamke ingawa katika Waraka wa Timotheo wanatajwa tu kuwa mashemasi wanaume tu. Kwa maana hiyo tunapata kuelewa kwamba Andiko la *1 TIMOTHEO 3:1-12*, Ingawa liliwataja maaskofu na mashemasi kuwa wanaume hapo , lakini hakumaishi kwa wanaume tu pekee yao , bali hata wanawake pia wanaweza kuwa mashemasi, na vilevile wachungaji (maaskofu) pia kwa msingi huo.
Ni muhimu kuyaelewa maandiko ya Biblia vizuri sio kila mahali andiko linapotaja jambo kwa upande mmoja linamainisha tu kwa upande mmoja pekee yake . Hapana. *Linaweza kutajwa kwa upande mmoja, lakini halikumainishi kuishia tu kwa upande mmoja, bali kwa pande zote mbili*. Kwa mfano , Yesu alisema, kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye moyoni mwake [ MATHAYO 5:27-28].
Sasa Swali la ufaham :- *Andiko hilo hapo linamgusa tu mwanaume kumtamani mwanamke ndio dhambi. Lakini Je, tuseme mwanamke naye akimtamani mwanaume kiuasherati, itakuwa siyo dhambi?* Kwa sababu tu eti Andiko hilo limemtaja tu mwanaume hapo? Jibu ni la!
Na kwa msingi huo huo hata kama Biblia imewataja wanaume kuwa ndio wawe maaskofu na mashemasi. Neno hilo halikuishia kumainisha tu kwa wanaume pekee yao bali hata kwa wanawake pia wanaweza kuwa wachungaji au maaskofu, mashemasi, mitume, manabii n.k.
Ni muhimu kufaham Biblia inasema katika *MATENDO 10:34-35:-*
*" Petro akafumbua kinywa chake, akasema, HAKIKA NATAMBUA YA KUWA MUNGU HANA UPENDELEO; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye. "*
Kusema kwamba mwanaume tu ndio anayepasa kuhubiri na kuwa Mchungaji lakini mwanamke hafai kwa lolote. Huo ni upendeleo. Mungu wetu hana upendeleo wa aina yoyote ile , kila mtu awe ni mwanaume au mwanamke bado Mungu anaweza kuwatumia wote sawasawa katika nafasi yoyote ile ya utumishi iwe ni uchungaji na kadhalika.
Ni muhimu kufaham katika suala la utumishi wowote mbele za Mungu. Mwanaume hawezi kujivuna na kujiinua kwamba yeye anastahili sana zaidi ya mwanamke. Katika imani ya wokovu iliyobeba utumishi ndani yake, sisi wote ni sawasawa mbele za Mungu. Hakuna mmoja aliye bora wa kujiinua juu zaidi ya mwingine. Biblia inasema katika
*1 WAKORINTHO 12:17-27:-*
*" BALI MUNGU AMEVITIA VIUNGO KILA KIMOJA KATIKA MWILI KAMA ALIVYOTAKA*. Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja. Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi. *Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi. Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana*. Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na *kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa;* ili kusiwe na faraka katika mwili, *bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe*. Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, *na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho*. Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake. Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza.............."
*YOHANA 6: 28-29:-*
*"Basi wakamwambia, Tufanyeje ili tupate KUZITENDA KAZI ZA MUNGU ? Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndiyo kazi ya Mungu, mmwamini yeye aliyetumwa na yeye."*
*WAGALATIA 3:26-29:-*
*"Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo. Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. HAPANA MTU MUME WALA MTU MKE. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu."*.
Maandiko hayo kwa ujumla wake yanatufundisha Mungu ndiye anaweza kuamua kumuweka mtu yoyote katika nafasi yoyote ya utumishi wa kazi ya huduma ya Mungu , huyu hivi na yule vile. Na kwa Mungu hakuna kigezo cha ubaguzi wowote wa jinsia katika nafasi yoyote ya kumtumikia .Na kwa maana hiyo *WANAUME NA WANAWAKE WOTE KWA PAMOJA WANAWEZA KUWA WAHUBIRI, WACHUNGAJI, MITUME N. k.*
Mwanaume huyu Akila na Mwanamke huyu Priska, mke na mume. Kwa pamoja wote wanatajwa kila mmoja wao katika kuhusika kuifanya kazi ya Mungu ya uchungaji waliokuwa nayo juu ya kanisa.
*[ WARUMI 16:3-4. ]*
Somo hili litaendelea sehemu ya pili........
πΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊ
Unakaribishwa pia kujiunga na group letu.
Mtumishi wa Mungu aliye hai.
*MWL, REV:- ODRICK BRYSON*
*SIMU (0759 386 988; 0717 591 466)*.
Whatsap group.
Email :- Odrick 16@gmail. Com.
*" KWELI YOTE YA NENO LA MUNGU ISIYOGOSHIWA"*.
[ 2 WAKORINTO 2:17 ]
πΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊ
*AU*
*KUWA MCHUNGAJI ❓*
( Sehemu ya kwanza )
<><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><>
Mistari muhimu ya kukumbuka:-
*1 WAKORINTHO 14:34-36:-*
*34 Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.*
*35 Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.*
36 Au je! Neno la Mungu lilitoka kwenu? Au kuwafikia ninyi peke yenu?
*1 TIMOTHEO 2:11-12:-*
11 Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.
*12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.*
πππππππππ
HII NI MADA YENYE UBISHI MKUBWA miongoni mwa vichwa vya watu wengi . Na maandiko hayo kwa kueleweka isivyo sahihi hutumiwa na baadhi ya watu wengi kujaribu kujenga hoja zao za kupinga kwamba mwanamke hana haki yoyote ya kuwa Mchungaji wala kusimama madhabahuni kuwahubiria watu kanisani.
Jambo hili limeleta mzozano mkubwa na mpasuko ndani ya makanisa mengi ya Mungu, kuhusu uhalali wa mwanamke kuhubiri madhabahuni na kuwa Mchungaji. Kuna mawazo ya positive na Negative, kuna wengine wanaona ni sahihi na kuna wengine kwao siyo sahihi kabisa .
Sasa basi ukweli na usahihi wa maandiko hayo ni upi basi? Je, ni sahihi kwamba mwanamke hatakiwi kuhubiri madhabahuni kanisani au kuwa Mchungaji ? Tatizo ni kwamba Maandiko hayo hayaeleweki vizuri kwa kwa wakristo wengi na hata baadhi ya wachungaji na Maaskofu, wanalifafanua hilo Andiko kwa maana potofu kabisa .
*NB:-*
Kuitwa Mtume, Nabii Askofu au Mchungaji n.k. Siyo kigezo kikubwa cha kwamba wewe unaielewa sana Biblia kwa usahihi wake. La asha ! Ndiomaana wako hata wachungaji wengine tena wengi tu ambao huyatafsiri maandiko isivyo na kuyapotosha kwa tamaa zao wenyewe.
MWALIMU MKUU WA BIBLIA NI ROHO MTAKATIFU; yeye ndiye aliyeyaleta maandiko hayo kwetu. Na hatuwezi sisi kuamua kuyatafsiri maandiko hayo vyovyote tu kama apendavyo mtu fulani kutafsiri. La Asha
*[ 2 PETRO 1:19-20 ]*.
Bali katika kanuni za kuyatafsiri maandiko, tunahitaji sana maongozi ya msaada wa Roho Mtakatifu mwenyewe katika kuyasoma na kuyaelewa maandiko vizuri na kuyatafsiri kwa usahihi wake. Neno la Biblia. Tunaweza kulifaham kwa kufunuliwa na Roho Mtakatifu pekee yake. Ndiomaana Yesu alisema *uliwaficha wenye hekima na Akili (Wasomi), ukawafunulia watoto wachanga (Watu wasio na elimu)*. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza mbele zako [ MATHAYO 11:25-26]. *"Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho Mtakatifu*. Maana Roho huchunguza yote hata mafumbo ya Mungu. Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, *bali Roho atokaye kwa Mungu makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu "*.
[1 WAKORINTHO 2:10-15].
Si hilo tu. Nikodemo alikuwa ni mwalimu mkuu wa chuo cha Torati. Na watu walimwamini sana katika Taifa la Israeli. Lakini Nikodemo alipoambiwa na Yesu maneno mepesi tu ya Mungu , na usomi wake wote, alishindwa kuyaelewa maana yake nini !! Sasa Yesu ambaye hakupita chuo chochote cha Theolojia, ikambidi amfundishe Nikodemo, mwalimu mkuu wa chuo cha Theolojia ya Torati.
[ YOHANA 3:1- 10 ]
Sisemi wala kupinga kwamba kusoma chuo cha Biblia ni kosa au ni vibaya, au ni dhambi. Hapana. Ni nini maana ya kuanza kukwambia hayo. Maana yangu ni hii kwamba :- Ondoa dhana potofu ukafikili kila mtu anayeitwa Mchungaji, Askofu au Mwanatheolojia fulani msomi anaielewa sana Biblia ki-maana. Ukiwa na mawazo hayo tu, utapotezwa na kudanganyika sana Mpendwa . Na Mungu huwa hatendi kazi kwa misingi hiyo. Mchungaji /Ev/ Mwanatheolojia huyo *Anaweza kuielewa Biblia kwa namna fulani tu ya akili hivi , lakini asiweze kabisa kuielewa Biblia kwa jinsi ya rohoni zaidi kwa ufunuo wa Roho Mtakatifu*. Na maana ya kweli ya maneno ya Biblia hutumbalikana kwa jinsi ya rohoni zaidi na sio kwa jinsi ya mwilini.
[ WAGALATIA 1:11-12 ; WAEFESO 1:17-19].
Hivyo ni vema zaidi tusiweke vipimo vyetu vya usomi kama kigezo cha kuitafsiri Biblia; bali tumuhitaji sana Roho wa Mungu ndio atuongoze katika kulitafsiri Neno lake Mungu.
*Je, ni halali Mwanamke kuhubiri au kuwa Mchungaji?*
Jibu :- Ni ndiyo kwa herufi kubwa.
Tutajifunza somo hili kwa kuligawa katika vipengele vinne. Ambavyo ni :-
*(1) HOJA POTOFU KUHUSU MWANAMKE KUTOKUWA MCHUNGAJI / MUHUBIRI.*
*(2) UHALALI WA MWANAMKE KUHUBIRI / KUFUNDISHA KANISANI*.
*(3) UHALALI WA MWANAMKE KUWA MCHUNGAJI*
*(4) UFAFANUZI WA ANDIKO LA 1 WAKORINTHO 14:34-35 NA 1 TIMOHEO 2:12*.
KIPENGELE NO:1
*HOJA POTOFU KUHUSU MWANAMKE KUTOKUWA MCHUNGAJI/ MUHUBILI*.
Ukiwasikia watu wengi wanaopinga mwanamke kuhubiri au kuwa Mchungaji. Mbali na kutumia Andiko la 1 Wakorintho 14:34-35 na 1 Timoheo 2:12-15 katika ufafanuzi wao .
Pia watajenga hoja yao nyingine ni kwamba *MWANAMKE NI KIUMBE DHAIFU* na hivyo wataeleza mengi tu katika kufafanua hoja yao hii.
Lakini mbele za Mungu, hoja ya mwanamke kutokuhubiri au kuwa Mchungaji kwa sababu eti ni kiumbe dhaifu. Hoja kama hii haikubaliki na wala haina maana yoyote. Kwa sababu Biblia inasema kwamba *Hao hao watu walio dhaifu machoni petu ndio Mungu anayewachagua kuwa watumishi wake*. Neno la Mungu linasema katika
*1WAKORINTHO 1: 26-29:-" Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; TENA MUNGU ALIVICHAGUA VITU VINYONGE VYA DUNIA NA VILIVYODHARAULIWA (WANAWAKE), naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu."*
Kwa maana hiyo ni muhimu kuzidi kuelewa na kufaham vizuri kwamba siku zote Mungu huwa hamchagui mtu yoyote kuwa mtumishi wake katika ngazi yoyote ya utumishi wa kihuduma kwa sababu tu ya kigezo cha jinsia yake kwamba ni kike au kiume. Hapana. Mungu hachagui mtu yoyote kwa kigezo cha sifa, umri, cheo au jinsia yake. Mungu huwa hatumikiwi wala kutenda kazi kwa misingi hiyo. Biblia inatuambia katika
*1 SAMWELI 16:7-10*:-
*7. Lakini BWANA akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. BWANA HAANGALII KAMA BINADAMU AANGALIAVYO; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali BWANA huutazama moyo.*
8. Ndipo Yese akamwita Abinadabu, akampitisha mbele ya Samweli. Naye *akasema, BWANA hakumchagua huyu*.
9. Ndipo Yese akampitisha Shama. *Naye akasema, wala BWANA hakumchagua huyu*.
10. Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli. *Samweli akamwambia Yese, BWANA hakuwachagua hawa*.
*WAFILIPI 3:3-4:-"Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, WALA HATUUTUMAINI MWILI. Walakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu ye yote akijiona kuwa anayo sababu ya kuutumainia mwili, mimi zaidi."*
Kwa sababu hiyo. Mungu katika mpango wake anaweza kumchagua mtu yoyote yule bila kujali sifa yake, umri wake au jinsia yake kwamba ni *mwanamke* au mwanaume , Mungu anaweza kumchagua awe mtumishi wake katika ngazi yoyote ya utumishi na tena akamtumia kwa viwango visivyo vya kawaida. Kwa hiyo sisi wanadamu hatupaswi kuamua kumpangia Mungu kwamba mwanamke hawezi kuwa Mchungaji au muhubiri. Kivipi !? *TUSILETE MFUMO-DUME NDANI YA KANISA LA MUNGU*. Hilo ni chaguo la Mungu sio la kwako wewe mwanadamu. Na kwa maana hiyo Mungu akiamua kumchagua mwanamke kuwa Mchungaji, Askofu, Mwinjilisti, mtume, Nabii n. k. Atakuwa hivyo Mchungaji, mtume, Nabii na kadhalika. Biblia inasema katika
*WARUMI 9:11-16*:-"
(kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, *ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye)*, aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo. Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia. Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha!
Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. *Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu."*
*WAEBRANIA 5:4:-" Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ILA YEYE AITWAYE NA MUNGU*, kama vile Haruni ".
Na kwa maana hiyo. Ngazi yoyote ya utumishi katika huduma mtu huwekwa na Mungu . Mungu akiamua kumwita mwanamke awe mchungaji, atakuwa ni Mchungaji tu na Mungu atajidhihirisha kwake kwa kumthibitisha kwamba yeye ndiye aliyemuita. *Wako wachungaji wanawake na wahubiri duniani ambao Mungu anawatumia kwa viwango vya juu sana katika huduma zao*. Hatuwezi kukanusha na kupinga utumishi wao kwa sababu tu ya kijinsia. *Yesu alisema kama hamniamini mimi, ziamini zile kazi , kwa kuwa kazi zenyewe zanishuhudia ya kwamba Baba Mungu amenituma*.
[ YOHANA 5:36; YOHANA 10:25, 36-38; YOHANA 14:10-12].
*HOJA YAO YA PILI.*
*Watasema hata maandiko yanamtaja kwamba mwanaume ndiye anayepaswa kuwa Mchungaji (Askofu). Uaskofu ni ngazi ya juu ya madaraka ya kichungaji*.
Na watatumia Andiko lao hili lifuatalo katika
*1 TIMOHEO 3:1-12:-*
1-7. Ni neno la kuaminiwa; *mtu akitaka kazi ya askofu*, atamani kazi njema. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, *MUME(MWANAUME) wa mke mmoja*, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha; mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)
Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.
Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.
8-12. *Vivyo hivyo mashemasi* na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana, si watu wanaotamani fedha ya aibu; wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia. Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; si wasingiziaji; watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.
*Mashemasi na wawe WAUME wa mke mmoja*, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao. Kwa maana watendao vema kazi ya shemasi hujipatia daraja nzuri, na ujasiri mwingi katika imani iliyo katika Kristo Yesu. "
Ni muhimu kuelewa vizuri Andiko hilo kwa kusema *mwanaume hapo ndiwe Askofu*. Haimanishi kwamba basi limemkataza Mwanamke asiwe mchungaji au Askofu. Hapana. Kwa sababu ukitazama mukadha mzima wa maelezo yote ya Andiko nzima, yameendelea kusema pia *" MASHEMASI NA WAWE WAUME wa mke mmoja "*. Sasa Je, kwa kusema hivyo tuseme Paulo Mtume hapo hakuwaruhusu pia wanawake wasiwe washemasi kwa sababu tu amewataja wanaume? Jibu ni hapana.
Tunaona pia walikuwepo *MASHEMASI WANAWAKE* ambao pia Paulo mtume aliwachagua katika kanisa. Ukisoma katika *WARUMI 16:1*, Biblia inasema:- *" Namkabidhi kwenu Fibi, Ndugu yetu, aliye muhudumu wa kanisa lililoko Kenkrea"*. Mstari huo katika Biblia ya kingereza ya *New International Version*, unasomeka hivi, *Romans 16:1:-" I commend to you our Sister Phoebe, a Servant (deaconess) of the church in Cenchrea"*.
Kwa hiyo tunaona hapo juu ya Shemasi Mwanamke ingawa katika Waraka wa Timotheo wanatajwa tu kuwa mashemasi wanaume tu. Kwa maana hiyo tunapata kuelewa kwamba Andiko la *1 TIMOTHEO 3:1-12*, Ingawa liliwataja maaskofu na mashemasi kuwa wanaume hapo , lakini hakumaishi kwa wanaume tu pekee yao , bali hata wanawake pia wanaweza kuwa mashemasi, na vilevile wachungaji (maaskofu) pia kwa msingi huo.
Ni muhimu kuyaelewa maandiko ya Biblia vizuri sio kila mahali andiko linapotaja jambo kwa upande mmoja linamainisha tu kwa upande mmoja pekee yake . Hapana. *Linaweza kutajwa kwa upande mmoja, lakini halikumainishi kuishia tu kwa upande mmoja, bali kwa pande zote mbili*. Kwa mfano , Yesu alisema, kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye moyoni mwake [ MATHAYO 5:27-28].
Sasa Swali la ufaham :- *Andiko hilo hapo linamgusa tu mwanaume kumtamani mwanamke ndio dhambi. Lakini Je, tuseme mwanamke naye akimtamani mwanaume kiuasherati, itakuwa siyo dhambi?* Kwa sababu tu eti Andiko hilo limemtaja tu mwanaume hapo? Jibu ni la!
Na kwa msingi huo huo hata kama Biblia imewataja wanaume kuwa ndio wawe maaskofu na mashemasi. Neno hilo halikuishia kumainisha tu kwa wanaume pekee yao bali hata kwa wanawake pia wanaweza kuwa wachungaji au maaskofu, mashemasi, mitume, manabii n.k.
Ni muhimu kufaham Biblia inasema katika *MATENDO 10:34-35:-*
*" Petro akafumbua kinywa chake, akasema, HAKIKA NATAMBUA YA KUWA MUNGU HANA UPENDELEO; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye. "*
Kusema kwamba mwanaume tu ndio anayepasa kuhubiri na kuwa Mchungaji lakini mwanamke hafai kwa lolote. Huo ni upendeleo. Mungu wetu hana upendeleo wa aina yoyote ile , kila mtu awe ni mwanaume au mwanamke bado Mungu anaweza kuwatumia wote sawasawa katika nafasi yoyote ile ya utumishi iwe ni uchungaji na kadhalika.
Ni muhimu kufaham katika suala la utumishi wowote mbele za Mungu. Mwanaume hawezi kujivuna na kujiinua kwamba yeye anastahili sana zaidi ya mwanamke. Katika imani ya wokovu iliyobeba utumishi ndani yake, sisi wote ni sawasawa mbele za Mungu. Hakuna mmoja aliye bora wa kujiinua juu zaidi ya mwingine. Biblia inasema katika
*1 WAKORINTHO 12:17-27:-*
*" BALI MUNGU AMEVITIA VIUNGO KILA KIMOJA KATIKA MWILI KAMA ALIVYOTAKA*. Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja. Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi. *Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi. Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana*. Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na *kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa;* ili kusiwe na faraka katika mwili, *bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe*. Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, *na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho*. Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake. Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza.............."
*YOHANA 6: 28-29:-*
*"Basi wakamwambia, Tufanyeje ili tupate KUZITENDA KAZI ZA MUNGU ? Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndiyo kazi ya Mungu, mmwamini yeye aliyetumwa na yeye."*
*WAGALATIA 3:26-29:-*
*"Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo. Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. HAPANA MTU MUME WALA MTU MKE. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu."*.
Maandiko hayo kwa ujumla wake yanatufundisha Mungu ndiye anaweza kuamua kumuweka mtu yoyote katika nafasi yoyote ya utumishi wa kazi ya huduma ya Mungu , huyu hivi na yule vile. Na kwa Mungu hakuna kigezo cha ubaguzi wowote wa jinsia katika nafasi yoyote ya kumtumikia .Na kwa maana hiyo *WANAUME NA WANAWAKE WOTE KWA PAMOJA WANAWEZA KUWA WAHUBIRI, WACHUNGAJI, MITUME N. k.*
Mwanaume huyu Akila na Mwanamke huyu Priska, mke na mume. Kwa pamoja wote wanatajwa kila mmoja wao katika kuhusika kuifanya kazi ya Mungu ya uchungaji waliokuwa nayo juu ya kanisa.
*[ WARUMI 16:3-4. ]*
Somo hili litaendelea sehemu ya pili........
πΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊ
Unakaribishwa pia kujiunga na group letu.
Mtumishi wa Mungu aliye hai.
*MWL, REV:- ODRICK BRYSON*
*SIMU (0759 386 988; 0717 591 466)*.
Whatsap group.
Email :- Odrick 16@gmail. Com.
*" KWELI YOTE YA NENO LA MUNGU ISIYOGOSHIWA"*.
[ 2 WAKORINTO 2:17 ]
πΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊπΊ
Monday, April 2, 2018
SOMO:JINSI YA KUIFAHAMU MIUJIZA YA MUNGU NA ISHARA ZA UONGO ZA MANABII WA UONGO (PART 1)
NENO LA MSINGI:
2 WATHESALONIKE 2:9:
"Yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa KUTENDA KWAKE SHETANI, KWA UWEZO WOTE, NA ISHARA NA AJABU ZA UONGO."
Katika somo la leo la Kanisa la Nyumbani, tunajifunza somo muhimu linaloambatana na majira tuliyo nayo ya nyakati za mwisho. Siku hizi, mahali pengi duniani ikiwamo Tanzania, kumezuka watu wa kila namna wakisema ni watumishi wa Mungu na kwamba wamepewa karama ya kutenda miujiza kwa ajili ya kuwasaidia watu. Kwa sababu hii, watu kila mahali wanamiminika kuwafuata, wakihitaji watoto au uponyaji mbalimbali wa mwili. Sehemu nyingine watu hao wanaodaiwa kuwa ni watumishi wa Mungu, wanatumia maji ya baraka kuponya; wengine wanatumia sanamu ya Bikira Maria; wengine wanawapeleka watu makaburini; wengine wanakwenda kupewa maji mahali inaposemekana alitokea Bikira Maria; wengine wanapewa madaftari ambamo humo wameandikiwa kwamba "Mungu" amesema watazaa mtoto wa kiume na wameandikiwa jina la kumwita, au mtoto wa kike na jina ambalo "Mungu" amemchagulia, na kupeleka madaftari hayo kila mara kuombewa na kukatazwa kwenda kliniki n.k. Wengine wamebeba "mimba" zilizotokana na maombezi ya watu hawa kwa miaka miwili bila kujifungua na kupata mateso makali mno. Wengine wameshuhudia kwamba wamepona kabisa baada ya kuhudumiwa na watu wa jinsi hiyo. Hapa ndipo penye mtego. Ili tusinaswe na mitego ya namna hii, Kanisa la Mungu linapaswa kufahamu Biblia inasema nini kuhusu Miujiza, Ishara na Ajabu za Mungu na zile za Shetani.
SHETANI ANA UWEZO WA KUFANYA MIUJIZA, ISHARA NA AJABU ZA UONGO
Miujiza kadhaa kwa kipimo kidogo cha uwezo ulio na mpaka. Wakati wana wa Israeli walipokuwa hawajatoka Misri, waganga na wachawi wa Farao, walifanya miujiza kwa uwezo wa shetani:
(a) Wachawi hawa walipozibwaga fimbo zao chini, ziligeuka kuwa nyoka kwa mfano wa muujiza alioufanya Mungu kwa kuwatumia Musa na Haruni [SOMA KUTOKA 7:8-12]
(b) Wachawi hawa walifanya muujiza wa kubadilisha maji kuwa damu kwa mfano wa muujiza alioufanya Mungu kwa kuwatumia Musa na Haruni [SOMA KUTOKA 7:19-22].
Unaona! Shetani ana uwezo wa kufanya miujiza na ishara. Biblia inasema katika:
UFUNUO WA YOHANA 16:14:
"Hizo ndizo roho za MASHETANI, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote, kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi."
Wakati wa dhiki Kuu, roho za Mashetani zitafanya ishara kubwa, hata kufanya moto kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu. [SOMA UFUNUO 13:11-13].
Lakini pamoja na ufahamu huu ulio nao sasa kwamba Shetani ana uwezo wa kufanya ishara na miujiza, bado inakupasa kufahamu jambo moja. Shetani ana mpaka katika uwezo wake wa kufanya miujiza. Hana uwezo wa Mungu wa KUTENDA MAMBO YOTE. Shetani hawezi kutenda mambo yote. Wachawi na waganga wa Farao ingawa walifanya miujiza tuliyoiona, hata hivyo walishindwa kufanya muujiza alioufanya Mungu kwa kuwatumia Musa na Haruni; pale walipoyabadilisha mavumbi ya nchi kuwa chawa. Wachawi hao waliposhindwa walikiri mbele ya Farao kwamba uwezo wa Mungu uko juu mno kuliko uwezo wao. [SOMA KUTOKA 8:16-19]. Wachawi na waganga wa Farao pia walishindwa kuzuia majipu yenye kufura yaliyotumbuka juu ya wanadamu wote wa Misri kutokana na mavumbi aliyoyarusha Musa hewani. Wachawi hao nao walipigwa majipu hayo [SOMA KUTOKA 9:8-11]. Fimbo ya Haruni ilizimeza fimbo za wachawi kudhihirisha uwezo wa Mungu ulivyo mkubwa mno kuliko wa majeshi yote ya shetani [SOMA KUTOKA 7:11-12].
ISHARA, AJABU NA MIUJIZA YA SHETANI WAKATI WOTE INA LENGO LA KUWAPOTEZA WANADAMU ILI WAANGAMIZWE
MATHAYO 24:24:
"Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu WAPATE KUWAPOTEZA, kama yamkini, hata walio wateule."
Ishara, ajabu na Miujiza ya Shetani ndiyo maana inaitwa pia "NGUVU YA UPOTEVU" kwa jinsi ambavyo miujiza hiyo ilivyo madanganyo ya udhalimu kwa hao wanaopotea ambao hawataki kuiamini kweli ya Mungu na kuokolewa na hatimaye kuzidi kuipenda kweli katika wokovu. Nguvu hiyo ya upotevu juu ya wanadamu, hatimaye inawafanya wanadamu hao kuhukumiwa na kwenda Jehanum ya moto. [SOMA 2 WATHESALONIKE 2:7-12]. Kwa sababu hii, Kanisa la Mungu lazima liwe macho na kufahamu waziwazi jinsi ya kuzifahamu ishara, ajabu na miujiza ya Shetani na kutofautisha na ile itokanayo na Mungu. Kwa maarifa haya, ni rahisi kuziepuka kazi zote za Shetani na manabii wake; na pia kuwasaidia wengine waliokwisha kunaswa.
ALAMA TISA ZINAZOAMBATANA NA ISHARA, AJABU NA MIUJIZA
INAYOTOKANA NA MUNGU
Kwa kuangalia alama hizi tisa zifuatazo, na kuhakikisha kwamba ZOTE ZINAKUWEPO; ndipo tunapoweza kuzitambua ishara, ajabu na miujiza inayotokana na Mungu na kuifahamu na kukwepa miujiza ya Shetani na manabii wake:
(1) Mtu anayetumiwa kufanya ishara, ajabu au miujiza na Mungu, inabidi awe ameamini au kuokolewa; akikiri mwenyewe wokovu ulio katika Kristo Yesu na kuushuhudia.
MARKO 16:17; "Na ishara hizi zitafuatana na hao WAAMINIO .....".
Mtu yeyote asiyeokolewa na kukiri wokovu na kuushuhudia, hawezi kufanya miujiza itokanayo na Mungu. Miujiza hiyo hutokana na Shetani.
(2) Huduma ya Uponyaji au Ishara yoyote inayotokana na Mungu lazima iambatane na Biblia au Neno la Mungu kwa kuwa Neno la Mungu ndiyo dawa ya Ugonjwa na tena ndilo linalofanya
miujiza. Huduma yoyote ya uponyaji wa miujiza isiyoambatana na Biblia au Neno la Mungu, inatokana na Shetani.
ZABURI 107:20: "HULITUMIA NENO LAKE, HUWAPONYA, huwatoa katika maangamizo yao."
MITHALI 4:20-22: "Mwanangu, SIKILIZA MANENO YANGU; ....UZISIKIE KAULI ZANGU .....MAANA NI UHAI kwa wale wazipatao, na AFYA YA MWILI WAO WOTE."
YOHANA 6:63: ".....MANENO HAYO NILIYOWAAMBIA niroho tena NI UZIMA."
(3) Huduma yoyote ya Uponyaji wa Miujiza inayotokana na Mungu, LAZIMA iambatane na kuhubiri Injili na kufundisha Neno la Mungu, Angalia maandiko:
(a) HUDUMA YA YESU:
(i) Kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao na vipofu kupata kuona tena, KULIAMBATANA na kuwahubiri maskini habari njema [SOMA LUKA 4:18].
(ii) Yesu alipokuwa akifundisha Neno la Mungu ndipo uweza wa Bwana ulipokuwapo kuponya:
LUKA 4:17:
"Ikawa siku zile mojawapo ALIKUWA AKIFUNDISHA .... NA UWEZA WA BWANA ULIKUWAPO APATE KUPONYA."
(4) YESU ALIPOWATUMA WANAFUNZI KUFANYA HUDUMA YA UPONYAJI
Wakati wote Yesu Kristo alipowatuma wanafunzi wake na kuwapa uwezo wa kuponya maradhi, au kuwaambia wapoze wagonjwa kwa miujiza; jambo hilo LILIAMBATANA na kutumwa kuhubiri au kuutangaza ufalme wa Mungu. Mambo haya mawili lazima yaende pamoja.
LUKA 9:1-2: "Akawaita wale Thenashara, akawapa uwezo na mamlaka juu ya pepo wote na kuponya maradhi. Akawatuma WAUTANGAZE UFALME WA MUNGU NA KUPOZAWAGONJWA."
LUKA 10:1-2, 9: "Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine,sabini, akawatuma wawili wawili .... Akawaambia ... WAPOZENI WAGONJWA waliomo, WAAMBIENI, UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA."
MATHAYO 10:7-8: "Na katika kuenenda kwenu, HUBIRINI,mkisema, Ufalme wa Mbinguni umekaribia. POZENI WAGONJWA, FUFUENI WAFU, TAKASENI WENYE UKOMA, TOENI PEPO; mmepata bure, toeni bure."
Katika kujifunza juu ya Huduma ya Yesu ya miujiza na uponyaji, na ile ambayo aliwapa wanafunzi wake; umeona kwamba kuponya wagonjwa kwa miujiza na kufanya ishara na ajabu zinazotokana na Mungu, LAZIMA kuambatane na kuhubiri Injili, na kuwaambia watu watubu dhambi zao na kuokolewa maana ufalme wa Mungu umekaribia. Ukimwona mtu anasema ni mtumishi wa Mungu na kwamba eti amepewa karama na Mungu kuponya wagonjwa, halafu akawa nyumbani kwake tu au ofisini kwake na watu wanamwijia kuponywa bila kuelezwa habari za kutubu na kuokolewa, ufahamu huyo ni nabii wa uongo, na anatumia NGUVU YA UPOTEVU ya Shetani kufanya ishara za uongo. Uponyaji wa Miujiza wa Mungu hauwi kama hospitali ambapo watu wanaenda kupewa vidonge tu bila kuhubiriwa Injili. Miujiza lazima iambatane na kuhubiri Injili. Mtu ukimsikia anasema yeye amepewa karama na Mungu kuponya wagonjwa tu, lakini hakupewa karama ya kuhubiri; hivyo kuhubiri amewaachia wengine, ujue huyo ni nabii wa uongo. Yeyote aliyepewa kufanya miujiza na Mungu, pia huyohuyo atahubiri Injili. Yesu, Petro, Paulo, Filipo na yeyote katika Biblia walifanya miujiza PAMOJA NA kuhubiri Injili.
Uponyaji wowote, muujiza wowote, au ishara yoyote inayofanywa kutokana na Mungu LAZIMA IFANYWE KWA JINA LA YESU SOMA: LUKA 10:17; MATENDO 4:30; MARKO 16:17; MATENDO 3:6; MATENDO 4:10; MATENDO 3:13, 16; MATENDO 16:18. Jina la Yesu, ndilo linalomtia mtu dhaifu, nguvu. Imani katika Yesu ndiyo inayoleta uzima [MATENDO 3:16]. Ukimwona mtu anayejiita mtumishi wa Mungu na kwamba anaombea wagonjwa, lakini halitumii Jina la Yesu ila anamtaja "Mungu" tu; ujue mtu huyo ni nabii wa uongo. Hakuna muujiza wowote wa Mungu pasipo kulitaja jina la Yesu! "PEPO WANATUTII KWA JINA LAKO", "KWA JINA LANGU WATATOA PEPO." Siyo kwa jina la Mungu au kwa kumtaja Mungu ila kwa jina la Yesu. LAZIMA Yesu atajwe katika kuufanya muujiza unaotokana na Mungu.
(5) Mtu anayetumiwa kufanya miujiza, ishara au ajabu na Mungu, hukusanya pamoja na Yesu, na kutumia miujiza kuliongeza Kanisa la Mungu kwa wale waaminio au wanaookolewa. Lengo la Mungu kutoa uwezo wa kufanya miujiza kwa watumishi wake, ni kuwafanya wasioamini waweze kuamini kwa kuziona nguvu za Mungu. Huduma yoyote ya miujiza isiyokuwa na lengo la kuwaongeza walioamini kwa Bwana Yesu au katika Kanisa la Mungu siyo huduma ya Mungu.
MATENDO 5:12,14:
"Na kwa mikono ya mitume zikafanyika ishara na maajabu mengi katika watu; ....walioamini wakazidi kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake".
Miujiza hutumika kukusanya watu na kuwaleta katika Kanisa ambalo kiongozi wake ni Yesu [SOMA PIA LUKA 11:23; MATHAYO 23:37; ZABURI 50:5].
INAENDELEA.................
KWA MAWASILIANO NAMI
SHUJAA Charles Mwaisemba
0712-054498/0759-420202
Limefundishwa na ASKOFU ZACHARY KAKOBE
NENO LA MSINGI:
2 WATHESALONIKE 2:9:
"Yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa KUTENDA KWAKE SHETANI, KWA UWEZO WOTE, NA ISHARA NA AJABU ZA UONGO."
Katika somo la leo la Kanisa la Nyumbani, tunajifunza somo muhimu linaloambatana na majira tuliyo nayo ya nyakati za mwisho. Siku hizi, mahali pengi duniani ikiwamo Tanzania, kumezuka watu wa kila namna wakisema ni watumishi wa Mungu na kwamba wamepewa karama ya kutenda miujiza kwa ajili ya kuwasaidia watu. Kwa sababu hii, watu kila mahali wanamiminika kuwafuata, wakihitaji watoto au uponyaji mbalimbali wa mwili. Sehemu nyingine watu hao wanaodaiwa kuwa ni watumishi wa Mungu, wanatumia maji ya baraka kuponya; wengine wanatumia sanamu ya Bikira Maria; wengine wanawapeleka watu makaburini; wengine wanakwenda kupewa maji mahali inaposemekana alitokea Bikira Maria; wengine wanapewa madaftari ambamo humo wameandikiwa kwamba "Mungu" amesema watazaa mtoto wa kiume na wameandikiwa jina la kumwita, au mtoto wa kike na jina ambalo "Mungu" amemchagulia, na kupeleka madaftari hayo kila mara kuombewa na kukatazwa kwenda kliniki n.k. Wengine wamebeba "mimba" zilizotokana na maombezi ya watu hawa kwa miaka miwili bila kujifungua na kupata mateso makali mno. Wengine wameshuhudia kwamba wamepona kabisa baada ya kuhudumiwa na watu wa jinsi hiyo. Hapa ndipo penye mtego. Ili tusinaswe na mitego ya namna hii, Kanisa la Mungu linapaswa kufahamu Biblia inasema nini kuhusu Miujiza, Ishara na Ajabu za Mungu na zile za Shetani.
SHETANI ANA UWEZO WA KUFANYA MIUJIZA, ISHARA NA AJABU ZA UONGO
Miujiza kadhaa kwa kipimo kidogo cha uwezo ulio na mpaka. Wakati wana wa Israeli walipokuwa hawajatoka Misri, waganga na wachawi wa Farao, walifanya miujiza kwa uwezo wa shetani:
(a) Wachawi hawa walipozibwaga fimbo zao chini, ziligeuka kuwa nyoka kwa mfano wa muujiza alioufanya Mungu kwa kuwatumia Musa na Haruni [SOMA KUTOKA 7:8-12]
(b) Wachawi hawa walifanya muujiza wa kubadilisha maji kuwa damu kwa mfano wa muujiza alioufanya Mungu kwa kuwatumia Musa na Haruni [SOMA KUTOKA 7:19-22].
Unaona! Shetani ana uwezo wa kufanya miujiza na ishara. Biblia inasema katika:
UFUNUO WA YOHANA 16:14:
"Hizo ndizo roho za MASHETANI, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote, kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi."
Wakati wa dhiki Kuu, roho za Mashetani zitafanya ishara kubwa, hata kufanya moto kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu. [SOMA UFUNUO 13:11-13].
Lakini pamoja na ufahamu huu ulio nao sasa kwamba Shetani ana uwezo wa kufanya ishara na miujiza, bado inakupasa kufahamu jambo moja. Shetani ana mpaka katika uwezo wake wa kufanya miujiza. Hana uwezo wa Mungu wa KUTENDA MAMBO YOTE. Shetani hawezi kutenda mambo yote. Wachawi na waganga wa Farao ingawa walifanya miujiza tuliyoiona, hata hivyo walishindwa kufanya muujiza alioufanya Mungu kwa kuwatumia Musa na Haruni; pale walipoyabadilisha mavumbi ya nchi kuwa chawa. Wachawi hao waliposhindwa walikiri mbele ya Farao kwamba uwezo wa Mungu uko juu mno kuliko uwezo wao. [SOMA KUTOKA 8:16-19]. Wachawi na waganga wa Farao pia walishindwa kuzuia majipu yenye kufura yaliyotumbuka juu ya wanadamu wote wa Misri kutokana na mavumbi aliyoyarusha Musa hewani. Wachawi hao nao walipigwa majipu hayo [SOMA KUTOKA 9:8-11]. Fimbo ya Haruni ilizimeza fimbo za wachawi kudhihirisha uwezo wa Mungu ulivyo mkubwa mno kuliko wa majeshi yote ya shetani [SOMA KUTOKA 7:11-12].
ISHARA, AJABU NA MIUJIZA YA SHETANI WAKATI WOTE INA LENGO LA KUWAPOTEZA WANADAMU ILI WAANGAMIZWE
MATHAYO 24:24:
"Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu WAPATE KUWAPOTEZA, kama yamkini, hata walio wateule."
Ishara, ajabu na Miujiza ya Shetani ndiyo maana inaitwa pia "NGUVU YA UPOTEVU" kwa jinsi ambavyo miujiza hiyo ilivyo madanganyo ya udhalimu kwa hao wanaopotea ambao hawataki kuiamini kweli ya Mungu na kuokolewa na hatimaye kuzidi kuipenda kweli katika wokovu. Nguvu hiyo ya upotevu juu ya wanadamu, hatimaye inawafanya wanadamu hao kuhukumiwa na kwenda Jehanum ya moto. [SOMA 2 WATHESALONIKE 2:7-12]. Kwa sababu hii, Kanisa la Mungu lazima liwe macho na kufahamu waziwazi jinsi ya kuzifahamu ishara, ajabu na miujiza ya Shetani na kutofautisha na ile itokanayo na Mungu. Kwa maarifa haya, ni rahisi kuziepuka kazi zote za Shetani na manabii wake; na pia kuwasaidia wengine waliokwisha kunaswa.
ALAMA TISA ZINAZOAMBATANA NA ISHARA, AJABU NA MIUJIZA
INAYOTOKANA NA MUNGU
Kwa kuangalia alama hizi tisa zifuatazo, na kuhakikisha kwamba ZOTE ZINAKUWEPO; ndipo tunapoweza kuzitambua ishara, ajabu na miujiza inayotokana na Mungu na kuifahamu na kukwepa miujiza ya Shetani na manabii wake:
(1) Mtu anayetumiwa kufanya ishara, ajabu au miujiza na Mungu, inabidi awe ameamini au kuokolewa; akikiri mwenyewe wokovu ulio katika Kristo Yesu na kuushuhudia.
MARKO 16:17; "Na ishara hizi zitafuatana na hao WAAMINIO .....".
Mtu yeyote asiyeokolewa na kukiri wokovu na kuushuhudia, hawezi kufanya miujiza itokanayo na Mungu. Miujiza hiyo hutokana na Shetani.
(2) Huduma ya Uponyaji au Ishara yoyote inayotokana na Mungu lazima iambatane na Biblia au Neno la Mungu kwa kuwa Neno la Mungu ndiyo dawa ya Ugonjwa na tena ndilo linalofanya
miujiza. Huduma yoyote ya uponyaji wa miujiza isiyoambatana na Biblia au Neno la Mungu, inatokana na Shetani.
ZABURI 107:20: "HULITUMIA NENO LAKE, HUWAPONYA, huwatoa katika maangamizo yao."
MITHALI 4:20-22: "Mwanangu, SIKILIZA MANENO YANGU; ....UZISIKIE KAULI ZANGU .....MAANA NI UHAI kwa wale wazipatao, na AFYA YA MWILI WAO WOTE."
YOHANA 6:63: ".....MANENO HAYO NILIYOWAAMBIA niroho tena NI UZIMA."
(3) Huduma yoyote ya Uponyaji wa Miujiza inayotokana na Mungu, LAZIMA iambatane na kuhubiri Injili na kufundisha Neno la Mungu, Angalia maandiko:
(a) HUDUMA YA YESU:
(i) Kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao na vipofu kupata kuona tena, KULIAMBATANA na kuwahubiri maskini habari njema [SOMA LUKA 4:18].
(ii) Yesu alipokuwa akifundisha Neno la Mungu ndipo uweza wa Bwana ulipokuwapo kuponya:
LUKA 4:17:
"Ikawa siku zile mojawapo ALIKUWA AKIFUNDISHA .... NA UWEZA WA BWANA ULIKUWAPO APATE KUPONYA."
(4) YESU ALIPOWATUMA WANAFUNZI KUFANYA HUDUMA YA UPONYAJI
Wakati wote Yesu Kristo alipowatuma wanafunzi wake na kuwapa uwezo wa kuponya maradhi, au kuwaambia wapoze wagonjwa kwa miujiza; jambo hilo LILIAMBATANA na kutumwa kuhubiri au kuutangaza ufalme wa Mungu. Mambo haya mawili lazima yaende pamoja.
LUKA 9:1-2: "Akawaita wale Thenashara, akawapa uwezo na mamlaka juu ya pepo wote na kuponya maradhi. Akawatuma WAUTANGAZE UFALME WA MUNGU NA KUPOZAWAGONJWA."
LUKA 10:1-2, 9: "Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine,sabini, akawatuma wawili wawili .... Akawaambia ... WAPOZENI WAGONJWA waliomo, WAAMBIENI, UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA."
MATHAYO 10:7-8: "Na katika kuenenda kwenu, HUBIRINI,mkisema, Ufalme wa Mbinguni umekaribia. POZENI WAGONJWA, FUFUENI WAFU, TAKASENI WENYE UKOMA, TOENI PEPO; mmepata bure, toeni bure."
Katika kujifunza juu ya Huduma ya Yesu ya miujiza na uponyaji, na ile ambayo aliwapa wanafunzi wake; umeona kwamba kuponya wagonjwa kwa miujiza na kufanya ishara na ajabu zinazotokana na Mungu, LAZIMA kuambatane na kuhubiri Injili, na kuwaambia watu watubu dhambi zao na kuokolewa maana ufalme wa Mungu umekaribia. Ukimwona mtu anasema ni mtumishi wa Mungu na kwamba eti amepewa karama na Mungu kuponya wagonjwa, halafu akawa nyumbani kwake tu au ofisini kwake na watu wanamwijia kuponywa bila kuelezwa habari za kutubu na kuokolewa, ufahamu huyo ni nabii wa uongo, na anatumia NGUVU YA UPOTEVU ya Shetani kufanya ishara za uongo. Uponyaji wa Miujiza wa Mungu hauwi kama hospitali ambapo watu wanaenda kupewa vidonge tu bila kuhubiriwa Injili. Miujiza lazima iambatane na kuhubiri Injili. Mtu ukimsikia anasema yeye amepewa karama na Mungu kuponya wagonjwa tu, lakini hakupewa karama ya kuhubiri; hivyo kuhubiri amewaachia wengine, ujue huyo ni nabii wa uongo. Yeyote aliyepewa kufanya miujiza na Mungu, pia huyohuyo atahubiri Injili. Yesu, Petro, Paulo, Filipo na yeyote katika Biblia walifanya miujiza PAMOJA NA kuhubiri Injili.
Uponyaji wowote, muujiza wowote, au ishara yoyote inayofanywa kutokana na Mungu LAZIMA IFANYWE KWA JINA LA YESU SOMA: LUKA 10:17; MATENDO 4:30; MARKO 16:17; MATENDO 3:6; MATENDO 4:10; MATENDO 3:13, 16; MATENDO 16:18. Jina la Yesu, ndilo linalomtia mtu dhaifu, nguvu. Imani katika Yesu ndiyo inayoleta uzima [MATENDO 3:16]. Ukimwona mtu anayejiita mtumishi wa Mungu na kwamba anaombea wagonjwa, lakini halitumii Jina la Yesu ila anamtaja "Mungu" tu; ujue mtu huyo ni nabii wa uongo. Hakuna muujiza wowote wa Mungu pasipo kulitaja jina la Yesu! "PEPO WANATUTII KWA JINA LAKO", "KWA JINA LANGU WATATOA PEPO." Siyo kwa jina la Mungu au kwa kumtaja Mungu ila kwa jina la Yesu. LAZIMA Yesu atajwe katika kuufanya muujiza unaotokana na Mungu.
(5) Mtu anayetumiwa kufanya miujiza, ishara au ajabu na Mungu, hukusanya pamoja na Yesu, na kutumia miujiza kuliongeza Kanisa la Mungu kwa wale waaminio au wanaookolewa. Lengo la Mungu kutoa uwezo wa kufanya miujiza kwa watumishi wake, ni kuwafanya wasioamini waweze kuamini kwa kuziona nguvu za Mungu. Huduma yoyote ya miujiza isiyokuwa na lengo la kuwaongeza walioamini kwa Bwana Yesu au katika Kanisa la Mungu siyo huduma ya Mungu.
MATENDO 5:12,14:
"Na kwa mikono ya mitume zikafanyika ishara na maajabu mengi katika watu; ....walioamini wakazidi kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake".
Miujiza hutumika kukusanya watu na kuwaleta katika Kanisa ambalo kiongozi wake ni Yesu [SOMA PIA LUKA 11:23; MATHAYO 23:37; ZABURI 50:5].
INAENDELEA.................
KWA MAWASILIANO NAMI
SHUJAA Charles Mwaisemba
0712-054498/0759-420202
Limefundishwa na ASKOFU ZACHARY KAKOBE
Sunday, March 18, 2018
MAMBO 12 YANAYOWEZA KUKUSAIDIA KUONGEZA NGUVU YA KUOMBA
Kuna mambo mengi sana yanayoweza kukusaidia ili nguvu yako ya maombi na kujibiwa kuongezeka. Tuangalie haya mambo 12:
1. TOBA NA UTAKASO: Kabla ya kuanza kuomba, omba toba kwa ajili yako na yule unayemuombea, jisafishe kwa Damu ya Yesu Kristo, na pia takasa eneo ambalo unaomba na kulikomboa katika ulimwengu wa roho. Nguvu yako ya kuomba inaweza kutegemea eneo ulipo. Hujawahi kuona kuna maeneo unaweza kuomba vizuri lakini kuna maeneo mengine ukishaenda nguvu ya kuomba haipo. Wengine akiwa kwenye kikundi cha maombi kanisani anakuwa na nguvu sana ya kuomba lakini akishafika nyumbani, nguvu yote inaisha. Unadhani shida ipo wapi? Eneo ni muhimu sana katika ulimwengu wa roho.
2. IJUE MAANA YA KUOMBA: Kuomba ni njia mojawapo ya kuzungumza na Mungu wetu. Unapomuita Mungu kwa kuomba anakusikiliza (Yeremia 29:12). “BWANA yu karibu kwa wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu”(Zaburi 145:18). Na njia mojawapo ya kumwita Mungu ni kwa njia ya maombi. “Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua”(Yeremia 33:3). Neno “mambo usiyoyajua” tukiliangalia kwa undani tunaona ni “mafunuo ya Mungu.” Kwa hiyo kuomba kunamfanya Mungu akupe mafunuo(revelation). Hivyo dumu katika kuomba (Wakolosai 4:2) kwani maombi ya mwenye haki yana nguvu (Yakobo 5:16).
3. MUDA: Muda/wakati ni muhimu sana katika ulimwengu wa roho hasa katika kuomba. Waefeso 5:16 inasema “tuukomboe wakati.” Maana yake wakati umetekwa na ibilisi. Moja ya silaha ambazo shetani anatumia kuua maombi ni kutumia muda. Akiweza kuuteka muda wako ameuwa maombi yako. Shetani alitumia sheria kujaribu kufunga muda wa maombi kwa kina Daniel siku 30 (Daniel 4). Kwa kuwa sheria sasa imeandikwa katika mioyo yetu Waebrania 10:16), muda unafungwa katika ulimwengu wa roho na matokeo yanatokea katika mwili.
Kuna watu ambao katika ulimwengu wa roho, shetani amefunga muda wao labda masaa 23 kwa siku. Maana yake katika siku huwezi kufanya maombi zaidi ya saa moja. Pia wengine muda wao umefungwa masaa 23 na dakika 45. Maana yake huwezi kuomba effectively zaidi ya dakika 15. Dakika 15 za mwanzo utaomba vizuri ila zikianza kuzidi, utaanza kupata uzito wa ajabu. Na kuna watu muda wao wa kuomba umefungwa masaa 24 kwa siku. Kwa huyu mtu hata kuomba dakika 5 ni kazi na ukianza tu kuomba, hapo hapo unaanza kusikia uzito. Kumbuka muda unafungwa katika ulimwengu wa roho, hivyo ukitaka kuukomboa, lazima uukomboe katika ulimwengu wa roho.
Na ukianza kufanya maombi ya kukomboa wakati sawa na Waefeso 5:16, shetani atakupiga vita. Lakini unaweza kuanza kukomboa kidogo kidogo. Mfano unashangaa ulikuwa huwezi kuomba nusu saa sasa unaweza. Baadae unaenda unaweza kuomba saa moja na kuendelea. Kama ulikuwa huwezi kuomba hata dakika 5 ni vigumu kuanza ghafla tu uweze kuomba kwa masaa 3 mfululizo. Maombi ya kuukomboa wakati ni maombi ya kufanya mara kwa mara.
4. KUWA NA NENO: Moja ya maombi ambayo yana nguvu sana ni maombi kwa kutumia neno la Mungu kwa imani. Unapokuwa unaomba kutumia neno la Mungu unamkumbusha Mungu kuwa yeye ni nani kwako. Neno la Mungu ni agano amefunga na wewe hivyo ukitumia neno unamkumbusha Mungu juu ya agano alilofunga na wewe. Mfano kama unahitaji uponyaji, unaweza kutumia mistari kama “kwa kupigwa kwake sisi tumepona” (Isaya 53:5) kwa imani. Mistari ya biblia itabaki kama mistari usipopata mafunuo kutoka kwa Roho Mtakatifu.
Unapotoa neno kama hilo kwa imani unampa Mungu kuachilia neno na kukujibu. “Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao” (Zaburi 107:20). Kwa hiyo unapomuomba Mungu kitu fulani hakupi hicho kitu ila anakupa neno lilibeba hicho kitu. Mfano ukiomba uponyaji anakupa neno lilibeba uponyaji na imani yako inakupa kupokea. Ukimuomba hela hakupi hela ila neno ambalo limebeba maarifa ya kupata hela. Ndo maana ni muhimu sana kuwa na neno la Mungu kwani yeye hujibu kwa ufasaha
5. OMBA MUNGU AKUPE MASIKIO YA KUSIKIA: Hiki kipengele kinaweza kuunganishwa na cha 4. Ili maombi yako yakue, unahitaji kuwa na neno la Kristo. Warumi 10:17 inasema “basi imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.” Kwa hiyo muombe Mungu akupe masikio ya kusikia ili uweze kusikia sauti ya neno lake. Siongelei masikio ya nje bali masikia ya ndani ambayo yanasikia kile ulichosikia. Matayo 13:13 inasema “wakisikia hawasikii wala kuelewa.” Kwa hiyo unaweza kusikia na usisikie kile ulichosikia. Lakini ukimuomba Mungu akupatie masikio ya kusikia itaongeza neno la Mungu ndani yako na kufanya maombi yako yawe na nguvu.
6. JIFUNZE KUUOMBEA MWILI WAKO: Kuomba ni jambo la rohoni na Mungu wetu anapenda tuwe tunaomba. Kwa sababu mwili na roho mara zote vinapingana (Wagalatia 5:17), mwili hautaki kabisa maombi. Kama unabisha siku moja fanya jaribio hili: Andaa maombi ya saa moja halafu mpigie simu rafiki yako mpendwa na umwambie mambo yote unataka kumwambia Mungu. Utakuta unaweza kumwambia rafiki yako kwa muda wa saa moja bila kuchoka. Sasa chukua hayo maombi halafu nenda mbele za Mungu kwa lengo la kuomba, utaona mwili unakugomea. Kwa hiyo ili uweze kuwa na maombi effective, lazima uushinde kwanza mwili.
Maandiko yanasema “Basi ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana” (Warumi 12:1). Kumbuka dunia, mwili, na shetani vinafanya kazi pamoja katika utatu wa uovu kwa ajili ya kupinga chochote kile cha Mungu kama kuomba. Hivyo kuwa na tabia ya kuuombea mwili wako kila siku. Kama unataka kuomba kwa saa moja, omba kwanza na kuukabidhi mwili wako kwa Mungu ili uweze kukubali maombi ya saa moja. Ukianza kuomba utaona mwili unakataa lakini unavyoendelea kuomba, eventually unaushinda na utashangaa unaomba kwa urahisi sana. Uombee mwili wako kila siku.
7. OMBA UPAKO WA KUOMBA: Maandiko yanasema Roho Mtakatifu ndiye anatusaidia kuomba (Warumi 8:26). Hivyo kila siku muombe Roho Mtakatifu akupe upako wa kukusaidia kuomba unapoanza kuomba. Hii ni sala ambayo unatakiwa uifanye kila siku kwani unahitaji Roho wa Mungu akusaidie katika maombi yako yote. Lakini unapoomba upako wa kuomba, muombe Roho Mtakatifu akuongoze kuomba katika kila kitu ili usiombe kwa tamaa zako, kitu ambacho kinaweza kumfanya Mungu asijibu maombi yako (Yakobo 4:3). Pia muombe Roho Mtakatifu akukumbushe neno (Yohana 14:26) la kukusaidia kuomba. Kumbuka kila unachotaka kufanya cha Mungu, kinahitaji upako wa Mungu. Wapendwa wengine huwa wanashindwa kuomba kutokana na kwamba wanajaribu kutumia nguvu zao kuomba.
8. OMBA KWA IMANI: Hiki ni kipengele muhimu kuliko vyote. Unapokuwa unaomba, weka imani yako kwa Yesu. Wengi wanaweka imani kwenye maombi, kwenye kupokea, kwenye kufunga, au kwenye kujibiwa. Unapoweka imani kwenye maombi halafu Mungu asipojibu, utaanza ku-question maombi yako. Na kama upo kwenye kikundi cha maombi utaanza kujiuliza juu ya hicho kikundi cha maombi na wengine wanaweza kuhama kikundi. Maana yake wanatoa imani ya maombi kwenye kundi moja na kuihamisha kwenye kundi jingine. Hii ni kuwa na “imani kwenye maombi” na siyo “kuomba kwa imani.” Lakini ukiweka imani yako kwa Yesu na usipojibiwaa maombi yako utamuuliza Yesu shida ipo wapi na atakujibu kwa kukupa neno lake. “Kwa sababu hii nawaambia, yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” (Marko 11:24). Unaweza kutumia msitari huo kumuuliza Mungu kwa nini hujapokea kile umeomba wakati amekuahidi utapokea.
9. ONGEZA NGUVU ITENDAYO KAZI NDANI YAKO: Ukisoma Waefeso 3:20 utaona kitu cha ajabu pale. Mungu anasema “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuwayazayo, na kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu.” Hapa Mungu anatuambia anajibu zaidi ya tunayoomba lakini pia anasema kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu. Hivyo moja ya njia ya kuongeza kujibiwa ni kuongeza nguvu ya Mungu ndani yako. Nguvu inayoongelewa ni upako wa Roho Mtakatifu kwani ndo nguvu pekee ambayo inatenda kazi ndani yetu. Ndo maana kama unataka kuongeza nguvu katika maombi yako huwezi kukwepa kujua aina mbali mbali za upako wa Roho Mtakatifu za kukusaidia wewe.
10. MATEGEMEO: Unapoenda mbele za Mungu kuomba unategema nini? Lazima uwe na mategemeo fulani katika maombi yako. Kama hutegemi chochote kutoka kwa Mungu, kwa nini unaomba? Kuna mambo tunatakiwa kuyategemea tunapokuwa tunaomba lakini kuna mambo hatutakiwi kuyategemea. Tegemeo kubwa juu ya maombi ni kwamba “na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake” (1 Yohana 3:22). Kwa hiyo lazima tuzishike kwanza amri za Mungu. Pia katika maombi utegemee kupata maarifa na roho ya ufaham (Wakolosai 1:9). Kuna mambo mengi zaidi ambayo unaweza kutegemea kwenye maombi. Lakini pia kuna mambo ambayo usiyategemee.
Kwanza usitegemee tu kila kitu kitakuwa rahisi. Omba kwa imani lakini usitegemee kuwa kila kitu kitaenda kirahisi kama unavyotaka wewe. “Kwa hiyo tulitaka kuja kwenu, naam, mimi Paulo, mara ya kwanza, na mara ya pili, na Shetani akatuzuia” (1 Wathesalonike 2:18). Daniel maombi yake yalizuiliwa siku 21 (Daniel 10:13). Kuna kipindi shetani anaweza kuzuia hivyo lazima ujue kuwa kuna wakati unapoomba unaenda kupambana. Uwe na imani ya kushinda lakini usiende kwa kutegemea kila kitu ni rahisi. Na level fulani ya maombi unatakiwa ku-bypass radar ya shetani. Njia mojawapo ni kunena kwa lugha (1 Wakorintho 14:2).
Pili usitegemee muujiza. Watu wengi wanapenda kuomba wakitegemea muujiza. Maandiko hayasemi tutaishi kwa muujiza bali kwa neno (Matayo 4:4). Sina maana kuwa maombi hayawezi kukuletea muujiza lakini usiwe unaenda mbele za Mungu kuomba kwa mategemeo ya muujiza. Miujiza ipo lakini kumbuka kila muujiza una sababu yake kuwepo na wakati wake kuwepo. Sababu na wakati wa kuwepo muujiza ikiondoka na muujiza huondoka (1 Waflme 17:14). Mungu mwenyewe anajua kipindi unahitaji muujiza. Hivyo mategemeo yako yasiwekwe kwenye muujiza bali yawekwe neno la Mungu. Kikubwa na cha msingi ni kwamba “twaenenda kwa imani, si kwa kuona” (2 Wakorintho 5:7).
11. PIMA NGUVU YA MAOMBI YAKO: Utajuaje kama maombi yako yana nguvu au hayana? Nguvu ya maombi haipimwi kwenye muda ambao unautumia kuomba bali kwenye matunda unayoyapata unapoomba. Maandiko yanasema “kwa matunda yao mtawatambua” (Matayo 7:16). Kwa lugha nyingine nguvu ya maombi yako inapimwa kwenye ongezeko la imani yako. Maombi yanatakiwa yakuze imani yako kwa Kristo na imani yako inapokua hata kujibiwa kwako na kiwango cha maisha kinaongezeka.
Lakini kumbuka kuwa “tunaishi kwa imani”(Warumi 1:17) na wala “hatuishi kwa maombi.” Jinsi nguvu yako ya maombi inavyongezeka ndivyo kujibiwa kutaongezeka na utaweza kuomba kwa muda mrefu. Ila kumbuka urefu wa maombi siyo nguvu ya maombi. Nguvu ya maombi iliyoko ndani yako siyo nguvu yako ila ni nguvu ya Roho Mtakatifu ifanyayo kazi ndani yako. Unaweza kuomba maombi marefu yasiyo na nguvu na pia unaweza kuomba maombi mafupi yakawa na nguvu. Hii inatege
12. MAOMBI YA KUFUNGA: Kuna level fulani ya maombi ambayo unahitaji kufunga na kuomba. Kuna mambo mengine ambayo Mungu hawezi kufanya mpaka umefunga na kuomba. “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga” (Matayo 17:21). Maombi ya kufunga ni maombi ambayo yana nguvu sana. Unapofunga unatakiwa uombe Roho Mtakatifu akuongoze mambo gani ufunge. Wengi huwa wanafunga kwa kuunyima mwili chakula na maji. Kwa mfano mtu hali asubuhi mpaka jioni.
Lakini wakati mwingine unatakiwa uinyine nafsi pia na hapa ndo huwa pagumu. Nafsi inalishwa kwa kuhisi, kuona, kusikia, kuonja na kunusa. Kwa wengine kufunga kwenye nafsi ni kugumu zaidi ya kufunga kwa mwili. Kuna watu wengine anaweza kufunga chakula siku mbili bila shida ila hawezi kuacha kutumia simu, kuangalia TV, au kusikia mziki. Wakati mwingine unaweza kufunga kwa ajili ya nafsi pia kwani lengo kubwa la kufunga nikujinyima vile mwili na nafsi inahitaji ili kuilisha roho. Soma Isaya 58 juu ya kufunga. Kuna sababu nyingi mtu anaweza kufunga na chache ni hizi:
Kufunga ili kutafuta msaada na mwongozo wa Mungu (Ezra 8:21—23).
Kufunga ili Mungu asikie maombi kilio na maombi yako (Esther 14:6; Nehemia 1:4—11).
Kufunga ili ushinde majaribu (Matayo 4).
Kufunga ili kuwa na upako wa huduma (Matendo 13:3).
MUHIMU: Maombi ni muhimu sana katika maisha ya kila anayeamini. Lakini usijaribu kuishi kwa maombi ila hakikisha unaishi kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu (Matayo 4:4). Watu wengi wameweka imani yao katika maombi kuliko katika neno. Matokeo yake wanakua katika maombi lakini hawakui katika kumjua Kristo kupitia neno lake.
Maombi yana nafasi yake lakini muhimu zaidi hakikisha una neno ili uweze kujenga imani yako. Ukisoma misingi 12 ya imani utakuta maombi siyo moja ya msingi. Umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi wanaweza kuomba kila siku lakini hawawezi kusoma neno kila siku? Umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi wakiwa wanaumwa au wanashida kitu cha kwanza watasema ni “ninahitaji maombi.” Ni wachache watasema “ninaumwa ninahitaji neno.” Maandiko yanatuambia Mungu hutuma neno la uponyaji (Zaburi 107:20). Hivyo unavyozidi kuongeza nguvu yako katika kuomba
Ubarikiwe!!
SHARE ZAIDI TAFADHALI
Kuna mambo mengi sana yanayoweza kukusaidia ili nguvu yako ya maombi na kujibiwa kuongezeka. Tuangalie haya mambo 12:
1. TOBA NA UTAKASO: Kabla ya kuanza kuomba, omba toba kwa ajili yako na yule unayemuombea, jisafishe kwa Damu ya Yesu Kristo, na pia takasa eneo ambalo unaomba na kulikomboa katika ulimwengu wa roho. Nguvu yako ya kuomba inaweza kutegemea eneo ulipo. Hujawahi kuona kuna maeneo unaweza kuomba vizuri lakini kuna maeneo mengine ukishaenda nguvu ya kuomba haipo. Wengine akiwa kwenye kikundi cha maombi kanisani anakuwa na nguvu sana ya kuomba lakini akishafika nyumbani, nguvu yote inaisha. Unadhani shida ipo wapi? Eneo ni muhimu sana katika ulimwengu wa roho.
2. IJUE MAANA YA KUOMBA: Kuomba ni njia mojawapo ya kuzungumza na Mungu wetu. Unapomuita Mungu kwa kuomba anakusikiliza (Yeremia 29:12). “BWANA yu karibu kwa wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu”(Zaburi 145:18). Na njia mojawapo ya kumwita Mungu ni kwa njia ya maombi. “Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua”(Yeremia 33:3). Neno “mambo usiyoyajua” tukiliangalia kwa undani tunaona ni “mafunuo ya Mungu.” Kwa hiyo kuomba kunamfanya Mungu akupe mafunuo(revelation). Hivyo dumu katika kuomba (Wakolosai 4:2) kwani maombi ya mwenye haki yana nguvu (Yakobo 5:16).
3. MUDA: Muda/wakati ni muhimu sana katika ulimwengu wa roho hasa katika kuomba. Waefeso 5:16 inasema “tuukomboe wakati.” Maana yake wakati umetekwa na ibilisi. Moja ya silaha ambazo shetani anatumia kuua maombi ni kutumia muda. Akiweza kuuteka muda wako ameuwa maombi yako. Shetani alitumia sheria kujaribu kufunga muda wa maombi kwa kina Daniel siku 30 (Daniel 4). Kwa kuwa sheria sasa imeandikwa katika mioyo yetu Waebrania 10:16), muda unafungwa katika ulimwengu wa roho na matokeo yanatokea katika mwili.
Kuna watu ambao katika ulimwengu wa roho, shetani amefunga muda wao labda masaa 23 kwa siku. Maana yake katika siku huwezi kufanya maombi zaidi ya saa moja. Pia wengine muda wao umefungwa masaa 23 na dakika 45. Maana yake huwezi kuomba effectively zaidi ya dakika 15. Dakika 15 za mwanzo utaomba vizuri ila zikianza kuzidi, utaanza kupata uzito wa ajabu. Na kuna watu muda wao wa kuomba umefungwa masaa 24 kwa siku. Kwa huyu mtu hata kuomba dakika 5 ni kazi na ukianza tu kuomba, hapo hapo unaanza kusikia uzito. Kumbuka muda unafungwa katika ulimwengu wa roho, hivyo ukitaka kuukomboa, lazima uukomboe katika ulimwengu wa roho.
Na ukianza kufanya maombi ya kukomboa wakati sawa na Waefeso 5:16, shetani atakupiga vita. Lakini unaweza kuanza kukomboa kidogo kidogo. Mfano unashangaa ulikuwa huwezi kuomba nusu saa sasa unaweza. Baadae unaenda unaweza kuomba saa moja na kuendelea. Kama ulikuwa huwezi kuomba hata dakika 5 ni vigumu kuanza ghafla tu uweze kuomba kwa masaa 3 mfululizo. Maombi ya kuukomboa wakati ni maombi ya kufanya mara kwa mara.
4. KUWA NA NENO: Moja ya maombi ambayo yana nguvu sana ni maombi kwa kutumia neno la Mungu kwa imani. Unapokuwa unaomba kutumia neno la Mungu unamkumbusha Mungu kuwa yeye ni nani kwako. Neno la Mungu ni agano amefunga na wewe hivyo ukitumia neno unamkumbusha Mungu juu ya agano alilofunga na wewe. Mfano kama unahitaji uponyaji, unaweza kutumia mistari kama “kwa kupigwa kwake sisi tumepona” (Isaya 53:5) kwa imani. Mistari ya biblia itabaki kama mistari usipopata mafunuo kutoka kwa Roho Mtakatifu.
Unapotoa neno kama hilo kwa imani unampa Mungu kuachilia neno na kukujibu. “Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao” (Zaburi 107:20). Kwa hiyo unapomuomba Mungu kitu fulani hakupi hicho kitu ila anakupa neno lilibeba hicho kitu. Mfano ukiomba uponyaji anakupa neno lilibeba uponyaji na imani yako inakupa kupokea. Ukimuomba hela hakupi hela ila neno ambalo limebeba maarifa ya kupata hela. Ndo maana ni muhimu sana kuwa na neno la Mungu kwani yeye hujibu kwa ufasaha
5. OMBA MUNGU AKUPE MASIKIO YA KUSIKIA: Hiki kipengele kinaweza kuunganishwa na cha 4. Ili maombi yako yakue, unahitaji kuwa na neno la Kristo. Warumi 10:17 inasema “basi imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.” Kwa hiyo muombe Mungu akupe masikio ya kusikia ili uweze kusikia sauti ya neno lake. Siongelei masikio ya nje bali masikia ya ndani ambayo yanasikia kile ulichosikia. Matayo 13:13 inasema “wakisikia hawasikii wala kuelewa.” Kwa hiyo unaweza kusikia na usisikie kile ulichosikia. Lakini ukimuomba Mungu akupatie masikio ya kusikia itaongeza neno la Mungu ndani yako na kufanya maombi yako yawe na nguvu.
6. JIFUNZE KUUOMBEA MWILI WAKO: Kuomba ni jambo la rohoni na Mungu wetu anapenda tuwe tunaomba. Kwa sababu mwili na roho mara zote vinapingana (Wagalatia 5:17), mwili hautaki kabisa maombi. Kama unabisha siku moja fanya jaribio hili: Andaa maombi ya saa moja halafu mpigie simu rafiki yako mpendwa na umwambie mambo yote unataka kumwambia Mungu. Utakuta unaweza kumwambia rafiki yako kwa muda wa saa moja bila kuchoka. Sasa chukua hayo maombi halafu nenda mbele za Mungu kwa lengo la kuomba, utaona mwili unakugomea. Kwa hiyo ili uweze kuwa na maombi effective, lazima uushinde kwanza mwili.
Maandiko yanasema “Basi ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana” (Warumi 12:1). Kumbuka dunia, mwili, na shetani vinafanya kazi pamoja katika utatu wa uovu kwa ajili ya kupinga chochote kile cha Mungu kama kuomba. Hivyo kuwa na tabia ya kuuombea mwili wako kila siku. Kama unataka kuomba kwa saa moja, omba kwanza na kuukabidhi mwili wako kwa Mungu ili uweze kukubali maombi ya saa moja. Ukianza kuomba utaona mwili unakataa lakini unavyoendelea kuomba, eventually unaushinda na utashangaa unaomba kwa urahisi sana. Uombee mwili wako kila siku.
7. OMBA UPAKO WA KUOMBA: Maandiko yanasema Roho Mtakatifu ndiye anatusaidia kuomba (Warumi 8:26). Hivyo kila siku muombe Roho Mtakatifu akupe upako wa kukusaidia kuomba unapoanza kuomba. Hii ni sala ambayo unatakiwa uifanye kila siku kwani unahitaji Roho wa Mungu akusaidie katika maombi yako yote. Lakini unapoomba upako wa kuomba, muombe Roho Mtakatifu akuongoze kuomba katika kila kitu ili usiombe kwa tamaa zako, kitu ambacho kinaweza kumfanya Mungu asijibu maombi yako (Yakobo 4:3). Pia muombe Roho Mtakatifu akukumbushe neno (Yohana 14:26) la kukusaidia kuomba. Kumbuka kila unachotaka kufanya cha Mungu, kinahitaji upako wa Mungu. Wapendwa wengine huwa wanashindwa kuomba kutokana na kwamba wanajaribu kutumia nguvu zao kuomba.
8. OMBA KWA IMANI: Hiki ni kipengele muhimu kuliko vyote. Unapokuwa unaomba, weka imani yako kwa Yesu. Wengi wanaweka imani kwenye maombi, kwenye kupokea, kwenye kufunga, au kwenye kujibiwa. Unapoweka imani kwenye maombi halafu Mungu asipojibu, utaanza ku-question maombi yako. Na kama upo kwenye kikundi cha maombi utaanza kujiuliza juu ya hicho kikundi cha maombi na wengine wanaweza kuhama kikundi. Maana yake wanatoa imani ya maombi kwenye kundi moja na kuihamisha kwenye kundi jingine. Hii ni kuwa na “imani kwenye maombi” na siyo “kuomba kwa imani.” Lakini ukiweka imani yako kwa Yesu na usipojibiwaa maombi yako utamuuliza Yesu shida ipo wapi na atakujibu kwa kukupa neno lake. “Kwa sababu hii nawaambia, yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” (Marko 11:24). Unaweza kutumia msitari huo kumuuliza Mungu kwa nini hujapokea kile umeomba wakati amekuahidi utapokea.
9. ONGEZA NGUVU ITENDAYO KAZI NDANI YAKO: Ukisoma Waefeso 3:20 utaona kitu cha ajabu pale. Mungu anasema “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuwayazayo, na kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu.” Hapa Mungu anatuambia anajibu zaidi ya tunayoomba lakini pia anasema kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu. Hivyo moja ya njia ya kuongeza kujibiwa ni kuongeza nguvu ya Mungu ndani yako. Nguvu inayoongelewa ni upako wa Roho Mtakatifu kwani ndo nguvu pekee ambayo inatenda kazi ndani yetu. Ndo maana kama unataka kuongeza nguvu katika maombi yako huwezi kukwepa kujua aina mbali mbali za upako wa Roho Mtakatifu za kukusaidia wewe.
10. MATEGEMEO: Unapoenda mbele za Mungu kuomba unategema nini? Lazima uwe na mategemeo fulani katika maombi yako. Kama hutegemi chochote kutoka kwa Mungu, kwa nini unaomba? Kuna mambo tunatakiwa kuyategemea tunapokuwa tunaomba lakini kuna mambo hatutakiwi kuyategemea. Tegemeo kubwa juu ya maombi ni kwamba “na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake” (1 Yohana 3:22). Kwa hiyo lazima tuzishike kwanza amri za Mungu. Pia katika maombi utegemee kupata maarifa na roho ya ufaham (Wakolosai 1:9). Kuna mambo mengi zaidi ambayo unaweza kutegemea kwenye maombi. Lakini pia kuna mambo ambayo usiyategemee.
Kwanza usitegemee tu kila kitu kitakuwa rahisi. Omba kwa imani lakini usitegemee kuwa kila kitu kitaenda kirahisi kama unavyotaka wewe. “Kwa hiyo tulitaka kuja kwenu, naam, mimi Paulo, mara ya kwanza, na mara ya pili, na Shetani akatuzuia” (1 Wathesalonike 2:18). Daniel maombi yake yalizuiliwa siku 21 (Daniel 10:13). Kuna kipindi shetani anaweza kuzuia hivyo lazima ujue kuwa kuna wakati unapoomba unaenda kupambana. Uwe na imani ya kushinda lakini usiende kwa kutegemea kila kitu ni rahisi. Na level fulani ya maombi unatakiwa ku-bypass radar ya shetani. Njia mojawapo ni kunena kwa lugha (1 Wakorintho 14:2).
Pili usitegemee muujiza. Watu wengi wanapenda kuomba wakitegemea muujiza. Maandiko hayasemi tutaishi kwa muujiza bali kwa neno (Matayo 4:4). Sina maana kuwa maombi hayawezi kukuletea muujiza lakini usiwe unaenda mbele za Mungu kuomba kwa mategemeo ya muujiza. Miujiza ipo lakini kumbuka kila muujiza una sababu yake kuwepo na wakati wake kuwepo. Sababu na wakati wa kuwepo muujiza ikiondoka na muujiza huondoka (1 Waflme 17:14). Mungu mwenyewe anajua kipindi unahitaji muujiza. Hivyo mategemeo yako yasiwekwe kwenye muujiza bali yawekwe neno la Mungu. Kikubwa na cha msingi ni kwamba “twaenenda kwa imani, si kwa kuona” (2 Wakorintho 5:7).
11. PIMA NGUVU YA MAOMBI YAKO: Utajuaje kama maombi yako yana nguvu au hayana? Nguvu ya maombi haipimwi kwenye muda ambao unautumia kuomba bali kwenye matunda unayoyapata unapoomba. Maandiko yanasema “kwa matunda yao mtawatambua” (Matayo 7:16). Kwa lugha nyingine nguvu ya maombi yako inapimwa kwenye ongezeko la imani yako. Maombi yanatakiwa yakuze imani yako kwa Kristo na imani yako inapokua hata kujibiwa kwako na kiwango cha maisha kinaongezeka.
Lakini kumbuka kuwa “tunaishi kwa imani”(Warumi 1:17) na wala “hatuishi kwa maombi.” Jinsi nguvu yako ya maombi inavyongezeka ndivyo kujibiwa kutaongezeka na utaweza kuomba kwa muda mrefu. Ila kumbuka urefu wa maombi siyo nguvu ya maombi. Nguvu ya maombi iliyoko ndani yako siyo nguvu yako ila ni nguvu ya Roho Mtakatifu ifanyayo kazi ndani yako. Unaweza kuomba maombi marefu yasiyo na nguvu na pia unaweza kuomba maombi mafupi yakawa na nguvu. Hii inatege
12. MAOMBI YA KUFUNGA: Kuna level fulani ya maombi ambayo unahitaji kufunga na kuomba. Kuna mambo mengine ambayo Mungu hawezi kufanya mpaka umefunga na kuomba. “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga” (Matayo 17:21). Maombi ya kufunga ni maombi ambayo yana nguvu sana. Unapofunga unatakiwa uombe Roho Mtakatifu akuongoze mambo gani ufunge. Wengi huwa wanafunga kwa kuunyima mwili chakula na maji. Kwa mfano mtu hali asubuhi mpaka jioni.
Lakini wakati mwingine unatakiwa uinyine nafsi pia na hapa ndo huwa pagumu. Nafsi inalishwa kwa kuhisi, kuona, kusikia, kuonja na kunusa. Kwa wengine kufunga kwenye nafsi ni kugumu zaidi ya kufunga kwa mwili. Kuna watu wengine anaweza kufunga chakula siku mbili bila shida ila hawezi kuacha kutumia simu, kuangalia TV, au kusikia mziki. Wakati mwingine unaweza kufunga kwa ajili ya nafsi pia kwani lengo kubwa la kufunga nikujinyima vile mwili na nafsi inahitaji ili kuilisha roho. Soma Isaya 58 juu ya kufunga. Kuna sababu nyingi mtu anaweza kufunga na chache ni hizi:
Kufunga ili kutafuta msaada na mwongozo wa Mungu (Ezra 8:21—23).
Kufunga ili Mungu asikie maombi kilio na maombi yako (Esther 14:6; Nehemia 1:4—11).
Kufunga ili ushinde majaribu (Matayo 4).
Kufunga ili kuwa na upako wa huduma (Matendo 13:3).
MUHIMU: Maombi ni muhimu sana katika maisha ya kila anayeamini. Lakini usijaribu kuishi kwa maombi ila hakikisha unaishi kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu (Matayo 4:4). Watu wengi wameweka imani yao katika maombi kuliko katika neno. Matokeo yake wanakua katika maombi lakini hawakui katika kumjua Kristo kupitia neno lake.
Maombi yana nafasi yake lakini muhimu zaidi hakikisha una neno ili uweze kujenga imani yako. Ukisoma misingi 12 ya imani utakuta maombi siyo moja ya msingi. Umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi wanaweza kuomba kila siku lakini hawawezi kusoma neno kila siku? Umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi wakiwa wanaumwa au wanashida kitu cha kwanza watasema ni “ninahitaji maombi.” Ni wachache watasema “ninaumwa ninahitaji neno.” Maandiko yanatuambia Mungu hutuma neno la uponyaji (Zaburi 107:20). Hivyo unavyozidi kuongeza nguvu yako katika kuomba
Ubarikiwe!!
SHARE ZAIDI TAFADHALI
Tuesday, March 6, 2018
Kati ya vitu ambavyo Mungu alimpa mwanadamu ni pamoja na KUCHAGUA! Kila kinachotokea kwako mara nyingi ni jinsi ulivyoamua kuchagua. Kuchagua kufaulu au kufeli, kuwa mtakatifu au mdhambi, kujiongoza au kuongozwa. Watu wengi tunashindwa kuchagua. Nimeamua kuchagua! Amua, anza!
*Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;*
KUM. 30:19.
✅Enzi na enzi maisha ya mwanadamu yaliongozwa na kuchagua; Adam na Hawa walichagua kutoisikia sauti ya Mungu wakamsikiliza nyoka *walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.*
MWA. 2:17
✅Esau alichagua kuitii njaa akauacha mbaraka wa mzaliwa wa kwanza *Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo Esau akaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.*
MWA. 25:34
✅Samson alichagua kumwambia siri Delila akapoteza agano lake kwa kumwambia adui siri za nguvu zake *Ndipo alipomwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akamwambia, Wembe haukupita juu ya kichwa changu kamwe; maana mimi nimekuwa Mnadhiri wa Mungu, tangu tumboni mwa mama yangu; nikinyolewa, ndipo nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu*
AMU. 16:17.
✅Mtume Paulo aliyaacha mambo ya faida kumfuata Kristo *Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.*
FLP. 3:7
✅Wanafunzi wa Yesu wanasema waliacha vyote *Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.*
MK. 10:28 πΉUchaguzi katika maisha yako unatengeneza kila kitu. Amua kuanza, amua kumtii Mungu, chagua ushindi. Jifunze kufanya maamuzi sahihi wakati wote.
*√Salamu kutoka makanisa ya PSAG ( Pentecostal Salvation Assemblies of God)!*Pastor Kyaruzi
*Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;*
KUM. 30:19.
✅Enzi na enzi maisha ya mwanadamu yaliongozwa na kuchagua; Adam na Hawa walichagua kutoisikia sauti ya Mungu wakamsikiliza nyoka *walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.*
MWA. 2:17
✅Esau alichagua kuitii njaa akauacha mbaraka wa mzaliwa wa kwanza *Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo Esau akaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.*
MWA. 25:34
✅Samson alichagua kumwambia siri Delila akapoteza agano lake kwa kumwambia adui siri za nguvu zake *Ndipo alipomwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akamwambia, Wembe haukupita juu ya kichwa changu kamwe; maana mimi nimekuwa Mnadhiri wa Mungu, tangu tumboni mwa mama yangu; nikinyolewa, ndipo nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu*
AMU. 16:17.
✅Mtume Paulo aliyaacha mambo ya faida kumfuata Kristo *Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.*
FLP. 3:7
✅Wanafunzi wa Yesu wanasema waliacha vyote *Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.*
MK. 10:28 πΉUchaguzi katika maisha yako unatengeneza kila kitu. Amua kuanza, amua kumtii Mungu, chagua ushindi. Jifunze kufanya maamuzi sahihi wakati wote.
*√Salamu kutoka makanisa ya PSAG ( Pentecostal Salvation Assemblies of God)!*Pastor Kyaruzi
Saturday, February 24, 2018
SEHEMU YA PILI
TAFSIRI KUHUSU WANA WA MUNGU
NA BINTI ZA WANADAMU (MW.6:1-4)
UTANGULIZI
Katika sehemu ya kwanza, nilitambulisha kambi mbili kuu za nadharia zinazokinzana kuhusu “wana wa Mungu” walioatajwa katika Mw.6:1-4 ni akina nani. Kambi moja inafundisha ni “malaika wa Mungu” walioasi kwa kuoana na binadamu na kuzaa watoto wa kinefili. Kambi ya pili inafundisha “wana wa Mungu” ni uzao wa Sethi” ambao walikengeuka na kuoana na binti za wanadamu wa “ukoo wa Kaini.”
Katika uchambuzi wa awali nilipingana na “nadharia ya malaika kuoana na binadamu”. Leo nawasilisha uchambuzi wa unaoangukia katika tafsiri ya pili inayofundisha kwamba “wana wa Mungu” sio malaika bali ni binadamu. Nitaanza kwa kuelezea chimbuko la historia ya ukoo wa uzao wa nyoka; pili chimbuko la historia ya ukoo wa “wana wa Mungu”, na tatu nitachambua kuhusu Mkengeuko Wa Maadili Ya Ndoa Kwa “Wana Wa Mungu” Kuoana Na Wasioamini. Karibuni:
1. Chimbuko La Historia Ya Ukoo Wa “Uzao Wa Nyoka”
Katika Mw.3:15 tunasoma ya kuwa Mungu mwenyewe ndiye alitabiri aina 2 tofauti za uzao pale alipotaja kuhusu “uadui” kati ya Uzao wa nyoka" na "uzao wa Mwanamke" (MW.3:15) Kutokana na “tamko la uadui” likawa ndilo chimbuko la “wana wa Mungu” na “binti za wanadamu” katika Mw.6:1-4.
Tukisoma katika Mwanzo Sura za 4 na 5 tunakuta ushahidi wa kihistoria ya watoto wa kwanza kiume wa Adamu, Kaini na Habili. Humo tunashuhudia jinsi ambavyo: “BWANA akamtakabali Habili na sadaka yake; lakini Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.” (Mw.4:4b-5) Baadaye tunamsoma Kaini anamwua Habili mdogo wake na kulaaniwa na Mungu: “Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;…” (Mw.4:11) Kuanzia hapo Kaini akawa ndio mwasisi wa “uzao wa nyoka”!
Kwa kupitia uzao wa Kaini tupata orodha ya watoto wake kuanzia Henoko, Iradi, Mehuyaeli, Methushaeli ambaye alimzaa Lameki. (Mw.17-18) Ni kwenye “ukoo wa uzao wa nyoka (Kaini) tunamkuta Lameki akianzisha utaratibu wa “ndoa za wake wengi”, kinyume cha maadili ya ndoa ya mke mmoja tangu Adamu na Hawa. (Mw.4:19)
Ushahidi mwingine unaothibitisha ya kuwa Kaini ndio “uzao wa nyoka uliolaaniwa”, ni pale mjukuu wake Lameki alipotoa kiapo hasi cha kuendeleza visasi vya mauaji kama babu yake: “ ….enyi wake za Lameki, sikilizeni usemi wangu; maana nimemwua mtu kwa kunitia jeraha; kijana kwa kunichubua; kama Kaini akilipiwa kisasi mara saba, hakika Lameki atalipiwa kisasi mara sabini na saba.” (Mw.4:23-24)
2. Chimbuko La Historia Ya Ukoo Wa “Wana Wa Mungu”
Baada ya ukoo wa “uzao wa nyoka” kupitia Kaini kuongezeka, tunamkuta Adamu amepata mtoto mwingine wa kiume akamwita jina lake Sethi. Sethi naye akamzaa Enoshi ambapo tusoma ya kuwa ndipo watu walipoanza kuliitia jina la BWANA.” (Mw.4:25-26)
Kwa mantiki hii, Sethi akawa ndiye baba wa ukoo wa “wana wa Mungu”! Ukoo wenyewe umeanishwa kwa kirefu katika Mwanzo 5:5-32 ukianzia kwa Sethi, Enoshi, Kenani, Mahalaleli, Yaredi, Henoko, Methusela, Lameki (si yule wa Kaini).
Ushahidi mwingine unaothibitisha ya kuwa “wana wa Mungu” ni “uzao wa Sethi” ni Nuhu ambaye ndiye aliyeonekana mtu wa haki wa kuendeleza ukoo safi wa wana wa Mungu baada ya hukumu ya Gharika: “Nuhu akapata neema machoni pa BWANA….Nuhu alikuwa mtu wa haki, mkamilifu katika vizazi vyake; Nuhu alikwenda pamoja na Mungu.”(Mw.6:8-9)
3. Mkengeuko Wa Maadili Ya Ndoa Kwa “Wana Wa Mungu” Kuoana Na Wasioamini
Sasa tuje kwenye kiini cha mjadala wa kisa cha Mw.6:1-4. Ushahidi wa kimaandiko katika kisa hiki unaonesha chimbuko la uharibifu sio “ndoa za malaika na binadamu” kama ilivyo kwa mtazamo wa nadharia husika.
Kiini cha mgogoro hapa ni “mkengeuko wa maadili ya ndoa” uliosababishwa na “Ukoo wa Sethi” ambao ndio “wana wa Mungu’ kuoana na binti za ukoo wa Kaini ambao hawakupaswa kuchangamana kifamilia. Mungu alikasirishwa na ukengeufu huu wa wana wa Sethi kuamua “kujitwalia wake waliowataka” kutoka ukoo wa Kaini na kuzaa nao watoto. Lakini sio hilo tu bali walivuka mipaka kwa kuacha utaratibu ndoa ya mke mmoja kwenda ndoa za wake wengi: “wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.” (Mw.6:2)
Msamiati wa neno “kujitwalia wake" kwa kiebrania ni laqah ukimaanisha “muungano wa kindoa” au “kujipatia mke”. Msamiati huo huo umetumika pia kwa “kujitwalia wake” kwa njia ya kuvunja maadili ya kimungu ya ndoa ya mke mmoja(Mw.2:23-24;MT.19:4-5) kwenda “ndoa za wake wengi” kama alivyofanya mjukuu wa Kaini:
“Lameki akajitwalia wake wawili, jina la kwa kwanza ni Ada, na jina la pili ni Sila.” (Mw.4:19) Hii ndiyo iliyomkasirisha Mungu kiasi cha kufupisha “kiwango cha ukomo wa kuishi”(Mw.6:3) duniani; na kisha kufutilia mbali kizazi chote cha binadamu na viumbe hai wote dunia nzima. (Mw.6:5-7)
Mpango wa Mungu tangu mwanzo ni kutunza ukoo safi wa uzao wa mwanamke ambao ungemzaa Yesu Kristo awe mkombozi wa ulimwengu. Ibilisi akamponda “adamu kisigino cha uasi” kwa kumwingia mzaliwa wa kwanza Kaini akalaaniwa. Ukoo wa Sethi ndio uliotegemewa kumleta mkombozi lakini nao pia ukaingiliwa na kukengeuka. Kwa neema akapatikana Nuhu na uzao wake.
Hata baada ya gharika tunaona Mungu aliendeleza msimamo wake mkali kwa “wana wa Mungu” wa kutokuingiliana kindoa na mataifa yenye kuamini miungu mingine: “Usije ukafanya agano na wenyeji wa nchi, watu wakaenda kufanya uzinzi na miungu yao, na kuitolea sadaka miungu yao; mtu mmoja akakuita ukaila sadaka yake. Ukawaoza wana wako binti zao, na binti zao wakaenda kufanya uzinzi na miungu yao, wakavuta wana wenu wafanye uzinzi na miungu yao.” (Kut.34:15-16)
“…..usifanye agano nao, wala kuwahurumia, wala usioane nao; binti yako usimpe mwanawe mume, na wala usimtwalie mwano mume binti yake. Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya BWANA juu yenu, naye atakuangamiza upesi..” (Kumb.7:2-4)
UFAFANUZI WA NYONGEZA KUHUSU
NDOA ZA MALAIKA NA BINADAMU
Kwenye makala iliyopita, baadhi ya wasomaji ninaowaheshimu sana waliuliza maswali kuhusu uhalali wa maelezo yangu ya kutokukubaliana na nadharia ya “wana wa Mungu” kuwa sio malaika. Walitaka kujua msamiati wa kiebrania wa “wana wa Mungu” unasemaje kama hauna maana ya malaika wa Mungu kuwa ndio wana wa Mungu. Na wengine wametaka kujua chimbuko la wanefili.
Naomba kuongeza ufafanuzi wa nyongeza katika kujibu maswali yaliyokwisha kuulizwa kama ifuatavyo: Tafsiri ya kiebrania ya “wana wa Mungu” ni bene ha'elohim. Katika Agano la Kale msamiati huu unapatikana sehemu kuu mbili kwenye Agano la kale. Ayu 6:1 na Ayub 2:1. Kwenye Ayu38:7 neno “ha” halipo. Katika sehemu hizo mbili tafsiri ya bene ha’elohim (wana wa Mungu) lilitumika kwa kwa malaika na mahali pengine kwa binadamu pia. (Hos.2:1; Kumb.14:1)
Lakini ukiuchunguza kwa makini muktadha wa maandiko ya kitabu cha Mwanzo utakuta hakuna mahali popote ambapo nadharia hii ya “wana wa Mungu” kuwa ni “malaika wa Mungu” imetajwa. Iwe ni katika Mwanzo au katika vitabu vyote vya Musa vya Kutoka, Hesabu, Walawi, na Kumbukumbu la Torati. Kwa maelezo mengine hii ni tafsiri ya kuazima kutoka kwenye vyanzo vingine ambavyo matumizi ya misamiati yake nayo haina uhusiano na tukio la ndoa zinazodaiwa kuwa za malaika na binadamu katika Mw.6:1-4)
Kana kwamba hii haikutosha, kuna uthibitisho wa kitafiti kwamba nadharia ya “malaika kuoana na binadamu” ilipata nguvu zaidi kutoka chanzo kingine cha taarifa cha “Kitabu cha Henoko” ambacho ndicho kimesimulia habari za ndoa za malaika kuacha enzi yao na kujitwalia wake za kibinandamu na kuzalisha watoto wa kinefili. Kitabu hicho kilitumiwa sana na baadhi ya wakristo maarufu wa karne za kwanza waliovutwa na taarifa zake wakiwemo akina Tertullian, Irenaeus, Origen, na Clement wa Alexandria.
Lakini baadaye Kitabu cha Henoko kilikataliwa kuingizwa kwenye orodha ya maandiko matakatifu ya Agano la Kale. Mojawapo ya sababu za kukataliwa ni paamoja na ukweli kwamba kitabu cha Henoko hakikuandikwa na Henoko mwenyewe. Hata hivyo baadhi ya wanazuoni wa tafsiri ya maandiko ya Kale waliendelea kutumia nukuu za kitabu hicho katika kutafsiri maandiko matakatifu.
CHUMBUKO LA WANEFILI
Watu wengi wameuliza maswali kuhusu wanefili ni akina nani na walitokea wapi! Katika sehemu ya kwanza nilijibu kwa sehemu ya kwamba, wanefili sio uzao wa kinachodaiwa ni mwingiliano wa kingono kati ya malaika na binadamu.
Jina la “wanefili” hali maana moja ya “majitu”. Pia kuna maneno tofauti ya kiebrania yenye tafsiri ya Wanefili. Kuna neno “naphal” likimaanisha “kuwashukia wengine” au “wenye kushambulia wengine” katika Yos 11:7; Ayu.1:15 na Yer.46:16. Neno la pili ni “palah” likiwa na maana “watu wasio wa kawaida” (extraordinary) Hii inamtaja mfalme mwenye nguvu nyingi mno za kuharibu kiasi cha kustaajabisha watu…(Dan.8:23-24)
Lakini pia wanefili lilitumika kwa binadamu wenye maumbile makubwa kama Goliati (1 Sa.17:4; 21:19-20) Sehemu nyingine ambapo tunasoma habari za wanefili ni wana wa Anaki katika Hes.13:22,28,33).
Jambo la kuzingatia hapa ni kuwa chimbuko la wanefili sio uzao wa ndoa za malaika na binadamu. Ni jamii ya watu waliotokana na uzao wa binadamu. Sasa kama hawa wanefili wa Wana wa Anaki walizaliwa na binadamu aliyeitwa Anaki, hali kadhalika na wanefili wa Mw 6:4. Nao walizaliwa na wana wa ukoo wa Kaini, na hasa kwa tabia yao ya ukatili wa kushambulia binadamu wengine katika jamii za wakati huo.
Pia kuna tofauti kati ya “wanefili” na “wana wa waliozaliwa kutokana na ndoa haramu za kibinadamu ambao wanaitwa “watu waliokuwa hodari na wenye sifa.”
Najua ya kwamba uchambuzi huu ni mgumu kwa baadhi. Nitakuwa tayari kujibu maswali yoyote yatakayoulizwa kutoka na uchambuzi wangu. Nitafurahi pia kupata maoni yako. Ubarikiwe sana.
Na askofu Sylvester Gamanywa
TAFSIRI KUHUSU WANA WA MUNGU
NA BINTI ZA WANADAMU (MW.6:1-4)
UTANGULIZI
Katika sehemu ya kwanza, nilitambulisha kambi mbili kuu za nadharia zinazokinzana kuhusu “wana wa Mungu” walioatajwa katika Mw.6:1-4 ni akina nani. Kambi moja inafundisha ni “malaika wa Mungu” walioasi kwa kuoana na binadamu na kuzaa watoto wa kinefili. Kambi ya pili inafundisha “wana wa Mungu” ni uzao wa Sethi” ambao walikengeuka na kuoana na binti za wanadamu wa “ukoo wa Kaini.”
Katika uchambuzi wa awali nilipingana na “nadharia ya malaika kuoana na binadamu”. Leo nawasilisha uchambuzi wa unaoangukia katika tafsiri ya pili inayofundisha kwamba “wana wa Mungu” sio malaika bali ni binadamu. Nitaanza kwa kuelezea chimbuko la historia ya ukoo wa uzao wa nyoka; pili chimbuko la historia ya ukoo wa “wana wa Mungu”, na tatu nitachambua kuhusu Mkengeuko Wa Maadili Ya Ndoa Kwa “Wana Wa Mungu” Kuoana Na Wasioamini. Karibuni:
1. Chimbuko La Historia Ya Ukoo Wa “Uzao Wa Nyoka”
Katika Mw.3:15 tunasoma ya kuwa Mungu mwenyewe ndiye alitabiri aina 2 tofauti za uzao pale alipotaja kuhusu “uadui” kati ya Uzao wa nyoka" na "uzao wa Mwanamke" (MW.3:15) Kutokana na “tamko la uadui” likawa ndilo chimbuko la “wana wa Mungu” na “binti za wanadamu” katika Mw.6:1-4.
Tukisoma katika Mwanzo Sura za 4 na 5 tunakuta ushahidi wa kihistoria ya watoto wa kwanza kiume wa Adamu, Kaini na Habili. Humo tunashuhudia jinsi ambavyo: “BWANA akamtakabali Habili na sadaka yake; lakini Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.” (Mw.4:4b-5) Baadaye tunamsoma Kaini anamwua Habili mdogo wake na kulaaniwa na Mungu: “Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;…” (Mw.4:11) Kuanzia hapo Kaini akawa ndio mwasisi wa “uzao wa nyoka”!
Kwa kupitia uzao wa Kaini tupata orodha ya watoto wake kuanzia Henoko, Iradi, Mehuyaeli, Methushaeli ambaye alimzaa Lameki. (Mw.17-18) Ni kwenye “ukoo wa uzao wa nyoka (Kaini) tunamkuta Lameki akianzisha utaratibu wa “ndoa za wake wengi”, kinyume cha maadili ya ndoa ya mke mmoja tangu Adamu na Hawa. (Mw.4:19)
Ushahidi mwingine unaothibitisha ya kuwa Kaini ndio “uzao wa nyoka uliolaaniwa”, ni pale mjukuu wake Lameki alipotoa kiapo hasi cha kuendeleza visasi vya mauaji kama babu yake: “ ….enyi wake za Lameki, sikilizeni usemi wangu; maana nimemwua mtu kwa kunitia jeraha; kijana kwa kunichubua; kama Kaini akilipiwa kisasi mara saba, hakika Lameki atalipiwa kisasi mara sabini na saba.” (Mw.4:23-24)
2. Chimbuko La Historia Ya Ukoo Wa “Wana Wa Mungu”
Baada ya ukoo wa “uzao wa nyoka” kupitia Kaini kuongezeka, tunamkuta Adamu amepata mtoto mwingine wa kiume akamwita jina lake Sethi. Sethi naye akamzaa Enoshi ambapo tusoma ya kuwa ndipo watu walipoanza kuliitia jina la BWANA.” (Mw.4:25-26)
Kwa mantiki hii, Sethi akawa ndiye baba wa ukoo wa “wana wa Mungu”! Ukoo wenyewe umeanishwa kwa kirefu katika Mwanzo 5:5-32 ukianzia kwa Sethi, Enoshi, Kenani, Mahalaleli, Yaredi, Henoko, Methusela, Lameki (si yule wa Kaini).
Ushahidi mwingine unaothibitisha ya kuwa “wana wa Mungu” ni “uzao wa Sethi” ni Nuhu ambaye ndiye aliyeonekana mtu wa haki wa kuendeleza ukoo safi wa wana wa Mungu baada ya hukumu ya Gharika: “Nuhu akapata neema machoni pa BWANA….Nuhu alikuwa mtu wa haki, mkamilifu katika vizazi vyake; Nuhu alikwenda pamoja na Mungu.”(Mw.6:8-9)
3. Mkengeuko Wa Maadili Ya Ndoa Kwa “Wana Wa Mungu” Kuoana Na Wasioamini
Sasa tuje kwenye kiini cha mjadala wa kisa cha Mw.6:1-4. Ushahidi wa kimaandiko katika kisa hiki unaonesha chimbuko la uharibifu sio “ndoa za malaika na binadamu” kama ilivyo kwa mtazamo wa nadharia husika.
Kiini cha mgogoro hapa ni “mkengeuko wa maadili ya ndoa” uliosababishwa na “Ukoo wa Sethi” ambao ndio “wana wa Mungu’ kuoana na binti za ukoo wa Kaini ambao hawakupaswa kuchangamana kifamilia. Mungu alikasirishwa na ukengeufu huu wa wana wa Sethi kuamua “kujitwalia wake waliowataka” kutoka ukoo wa Kaini na kuzaa nao watoto. Lakini sio hilo tu bali walivuka mipaka kwa kuacha utaratibu ndoa ya mke mmoja kwenda ndoa za wake wengi: “wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.” (Mw.6:2)
Msamiati wa neno “kujitwalia wake" kwa kiebrania ni laqah ukimaanisha “muungano wa kindoa” au “kujipatia mke”. Msamiati huo huo umetumika pia kwa “kujitwalia wake” kwa njia ya kuvunja maadili ya kimungu ya ndoa ya mke mmoja(Mw.2:23-24;MT.19:4-5) kwenda “ndoa za wake wengi” kama alivyofanya mjukuu wa Kaini:
“Lameki akajitwalia wake wawili, jina la kwa kwanza ni Ada, na jina la pili ni Sila.” (Mw.4:19) Hii ndiyo iliyomkasirisha Mungu kiasi cha kufupisha “kiwango cha ukomo wa kuishi”(Mw.6:3) duniani; na kisha kufutilia mbali kizazi chote cha binadamu na viumbe hai wote dunia nzima. (Mw.6:5-7)
Mpango wa Mungu tangu mwanzo ni kutunza ukoo safi wa uzao wa mwanamke ambao ungemzaa Yesu Kristo awe mkombozi wa ulimwengu. Ibilisi akamponda “adamu kisigino cha uasi” kwa kumwingia mzaliwa wa kwanza Kaini akalaaniwa. Ukoo wa Sethi ndio uliotegemewa kumleta mkombozi lakini nao pia ukaingiliwa na kukengeuka. Kwa neema akapatikana Nuhu na uzao wake.
Hata baada ya gharika tunaona Mungu aliendeleza msimamo wake mkali kwa “wana wa Mungu” wa kutokuingiliana kindoa na mataifa yenye kuamini miungu mingine: “Usije ukafanya agano na wenyeji wa nchi, watu wakaenda kufanya uzinzi na miungu yao, na kuitolea sadaka miungu yao; mtu mmoja akakuita ukaila sadaka yake. Ukawaoza wana wako binti zao, na binti zao wakaenda kufanya uzinzi na miungu yao, wakavuta wana wenu wafanye uzinzi na miungu yao.” (Kut.34:15-16)
“…..usifanye agano nao, wala kuwahurumia, wala usioane nao; binti yako usimpe mwanawe mume, na wala usimtwalie mwano mume binti yake. Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya BWANA juu yenu, naye atakuangamiza upesi..” (Kumb.7:2-4)
UFAFANUZI WA NYONGEZA KUHUSU
NDOA ZA MALAIKA NA BINADAMU
Kwenye makala iliyopita, baadhi ya wasomaji ninaowaheshimu sana waliuliza maswali kuhusu uhalali wa maelezo yangu ya kutokukubaliana na nadharia ya “wana wa Mungu” kuwa sio malaika. Walitaka kujua msamiati wa kiebrania wa “wana wa Mungu” unasemaje kama hauna maana ya malaika wa Mungu kuwa ndio wana wa Mungu. Na wengine wametaka kujua chimbuko la wanefili.
Naomba kuongeza ufafanuzi wa nyongeza katika kujibu maswali yaliyokwisha kuulizwa kama ifuatavyo: Tafsiri ya kiebrania ya “wana wa Mungu” ni bene ha'elohim. Katika Agano la Kale msamiati huu unapatikana sehemu kuu mbili kwenye Agano la kale. Ayu 6:1 na Ayub 2:1. Kwenye Ayu38:7 neno “ha” halipo. Katika sehemu hizo mbili tafsiri ya bene ha’elohim (wana wa Mungu) lilitumika kwa kwa malaika na mahali pengine kwa binadamu pia. (Hos.2:1; Kumb.14:1)
Lakini ukiuchunguza kwa makini muktadha wa maandiko ya kitabu cha Mwanzo utakuta hakuna mahali popote ambapo nadharia hii ya “wana wa Mungu” kuwa ni “malaika wa Mungu” imetajwa. Iwe ni katika Mwanzo au katika vitabu vyote vya Musa vya Kutoka, Hesabu, Walawi, na Kumbukumbu la Torati. Kwa maelezo mengine hii ni tafsiri ya kuazima kutoka kwenye vyanzo vingine ambavyo matumizi ya misamiati yake nayo haina uhusiano na tukio la ndoa zinazodaiwa kuwa za malaika na binadamu katika Mw.6:1-4)
Kana kwamba hii haikutosha, kuna uthibitisho wa kitafiti kwamba nadharia ya “malaika kuoana na binadamu” ilipata nguvu zaidi kutoka chanzo kingine cha taarifa cha “Kitabu cha Henoko” ambacho ndicho kimesimulia habari za ndoa za malaika kuacha enzi yao na kujitwalia wake za kibinandamu na kuzalisha watoto wa kinefili. Kitabu hicho kilitumiwa sana na baadhi ya wakristo maarufu wa karne za kwanza waliovutwa na taarifa zake wakiwemo akina Tertullian, Irenaeus, Origen, na Clement wa Alexandria.
Lakini baadaye Kitabu cha Henoko kilikataliwa kuingizwa kwenye orodha ya maandiko matakatifu ya Agano la Kale. Mojawapo ya sababu za kukataliwa ni paamoja na ukweli kwamba kitabu cha Henoko hakikuandikwa na Henoko mwenyewe. Hata hivyo baadhi ya wanazuoni wa tafsiri ya maandiko ya Kale waliendelea kutumia nukuu za kitabu hicho katika kutafsiri maandiko matakatifu.
CHUMBUKO LA WANEFILI
Watu wengi wameuliza maswali kuhusu wanefili ni akina nani na walitokea wapi! Katika sehemu ya kwanza nilijibu kwa sehemu ya kwamba, wanefili sio uzao wa kinachodaiwa ni mwingiliano wa kingono kati ya malaika na binadamu.
Jina la “wanefili” hali maana moja ya “majitu”. Pia kuna maneno tofauti ya kiebrania yenye tafsiri ya Wanefili. Kuna neno “naphal” likimaanisha “kuwashukia wengine” au “wenye kushambulia wengine” katika Yos 11:7; Ayu.1:15 na Yer.46:16. Neno la pili ni “palah” likiwa na maana “watu wasio wa kawaida” (extraordinary) Hii inamtaja mfalme mwenye nguvu nyingi mno za kuharibu kiasi cha kustaajabisha watu…(Dan.8:23-24)
Lakini pia wanefili lilitumika kwa binadamu wenye maumbile makubwa kama Goliati (1 Sa.17:4; 21:19-20) Sehemu nyingine ambapo tunasoma habari za wanefili ni wana wa Anaki katika Hes.13:22,28,33).
Jambo la kuzingatia hapa ni kuwa chimbuko la wanefili sio uzao wa ndoa za malaika na binadamu. Ni jamii ya watu waliotokana na uzao wa binadamu. Sasa kama hawa wanefili wa Wana wa Anaki walizaliwa na binadamu aliyeitwa Anaki, hali kadhalika na wanefili wa Mw 6:4. Nao walizaliwa na wana wa ukoo wa Kaini, na hasa kwa tabia yao ya ukatili wa kushambulia binadamu wengine katika jamii za wakati huo.
Pia kuna tofauti kati ya “wanefili” na “wana wa waliozaliwa kutokana na ndoa haramu za kibinadamu ambao wanaitwa “watu waliokuwa hodari na wenye sifa.”
Najua ya kwamba uchambuzi huu ni mgumu kwa baadhi. Nitakuwa tayari kujibu maswali yoyote yatakayoulizwa kutoka na uchambuzi wangu. Nitafurahi pia kupata maoni yako. Ubarikiwe sana.
Na askofu Sylvester Gamanywa
Thursday, February 15, 2018
Somo: UPONYAJI WA NAFSI ILIYOUMIZWA.
Mnenaji: Mwalimu Dickson Cornel Kabigumila.
Tukio: Semina Maalum ya Wadada
Tarehe: 14/02/2016
Utangulizi
⚡Nafsi imegawanyika katika sehem kuu tatu.
1)Hisia (Emotions & Feelings)
2)Maamuzi na machaguo (choices and decisions)
3)Akili (Intellect part)
Na katika somo hili tunajifunza kuhusu hisia.
1)HISIA
Hisia zipo ndani ya mtu tayari na zinaamka zikipata reaction kutoka nje.
Kuna aina mbili za hisia
a) Positive feelings
mfano: furaha, amani, kushangilia nk
b) Negative feelings
mfano: kulia, huzuni, uchungu nk
Vyote hivi vipo ndani ya mtu tayari lakini hadi vipate reaction kutoka nje ndio vitaonekana.
Hisia zinatokana na taarifa kutoka kwenye milango mitano ya ufahamu.
Yaani: Hata Mungu aliyetuumba sisi kwa sura na mfano wake ana hisia hizi za aina mbili:
i)Hasi
Mfano: "Hasira ya Bwana ikawaka"
Au "Mimi ni Mungu mwenye wivu"
Ama
"Wala msimhuzunishe Roho mtakatifu"
Hizi hisia hata Baba yetu anazo lakini anajua namna ya kuzicontrol!
ii) Chanya
"Mungu ni pendo"
Au
"Furaha ya Bwana ni nguvu yetu" ikiwa na maana anafurahi pia.
Lakini anajua namna ya kuzitawala hisia zake.
Hivyo basi, si tatizo kuwa na hisia chanya.
Bali hisia hasi usipojua namna ya kuzitawala na kuzimilki zitakuharibia maisha na watu wengine wanaokuzunguka.
Kumbuka: Hauwezi kuomba ili hasira isiweko kabisa ndani yako, ila unaweza kuomba "hasira isikutawale" (Waefeso 4:26).
Na ni wajibu wako kumnyima nafasi Ibilisi kukulisha taarifa mbaya na kukujeruhi ili kuamsha "hisia hasi" ndani yako ili ufanye dhambi na matukio mabaya!
Jambo jingine la muhimu kujua:
Vichocheo vinavyoamsha hisia hasi (hasira, uchungu, majeraha ya nafsi, visasi) yanakuja kupitia MILANGO MITANO YA FAHAMU.
Unachoona
Unachosikia
Unachogusa/hisi
Unachonusa
Unacholamba
Kama si kizuri, HISIA HASI zitaamka ndani yako na unaweza kufanya mambo ya ajabu.
Jiandae, uko duniani, utaona mengi mabaya ya kuumiza, utasikia taarifa mbaya, utahisi, utagusa na hata kunusa vitu vinavyokera na kuboa.
Mwitikio wako ndio utakaoamua nini utafanya na nini kitajengeka ndani yako.
Ili kushinda hisia mbaya, na majeraha ya nafsi tunapaswa tujue kanuni za Kibiblia za kutawala milango yetu mitano ya fahamu na kila kinachoingia ndani yetu kupitia hiyo!
kwahyo ili tuweze kujicontrol kwenye negative feelings zisituaffect maisha yetu na kuona hatuna sababu yoyote ya kuishi kwasababu ya tarifa uliyosikia au kuona ikaaamsha hisia zako tunapaswa kuwa na taarifa nyingi za neno la Mungu ili ziweze kubadilisha mazingira ya nje.
Hasira, Wivu, huzuni, uchungu vyote hivi vinapaswa viwe controlled na neno la Mungu.
Mungu akusaidie kutembea juu ya kila changamoto kutokana na wingi wa neno lililojaa ndani yako na lenye uvuvio wa Roho Mtakatifu..
❤❤ vitu viwili vinavyokaa karibu na moyo wa mtu
a) Yesu (neno)
Ufunuo 3:20 msaada ambao upo muda wowote.
ukimkataa Shetani then umemkubali Yesu
b) Dhambi
Mwanzo 4:7
ukimkubali shetani then umemkataa Yesu.
Yesu yuko karibu na moyo wako kwa mujibu wa Ufunuo 3:20, akisubiri umpe nafasi akusaidie.
Lakini pia dhambi iko mlangoni kwa moyo wako ikisubiri uliache Neno na agizo la Mungu iingie ndani yako.
Kama ilivyokuwa kwa Kaini (Mwanzo 4:7-8)
Ni wajibu wako kuruhusu nini kiingie na kipi kisiingie MOYONI MWAKO hasa UNAPOPATA TAARIFA MBAYA kutoka kwenye mazingira yako, watu wako, ndugu, mme, mke, watoto, biashara yako nakadhalika.
Ayubu alipopata TAARIFA MBAYA kuhusu wanae, mifugo, mali zake na hata afya yake, HAKUTENDA DHAMBI WALA KUMUWAZIA MUNGU KWA UPUMBAVU (Ayubu 1:22).
Alijua namna ya KUKABILI TAARIFA KUTOKA NJE.
Biblia inasema alichofanya ni "KUMSIFU MUNGU" akisema "JINA LA BWANA LIBARIKIWE"
Ni wajibu wako kujipanga kwa Neno, kwa kumuomba Mungu, na kupata nguvu ya kukabili kila HABARI MBAYA.
"Mwenye haki HATAOGOPA HABARI MBAYA, MOYO WAKE UIMARA UKIMTUMAINI BWANA"
(Zaburi 112:6-7).
Kadri ambavyo UNAKABIDHI MOYO WAKO KWA BWANA... UNA UHAKIKA WA KUTOTETEREKA HABARI MBAYA NA MABAYA YAKITOKEA.
Lakini kadri unavyokuwa unaombea vitu na maisha yako (unavikabidhi kwa Bwana kama Ayubu alivyokuwa akifanya ibada kwa ajili ya wanae na kuwatolea sadaka), unajikuta UNAJUA MUNGU YUKO KAZINI, BILA KUJALI NINI KINAKUTOKEA!
Waebrania 5:7 " Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule,awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu."
hapa tunaona Yesu pia alilia.
wanawake na mabinti wengi huwa tukiumia ni wepesi sana kulia...
Yaan haijalishi umeumizwa kiasi gani usiseme siwezi kuomba nooooo nenda mbele za Mungu kwa machozi na kulia Mungu anasikia aisee.
Stephano pia alilia.
1 Peter 5:7
" huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.
⚡Mungu anajishughulisha sana kwa mambo yetu sio mambo yake ni yetu kwahyo kazi yetu ni kumtika yeye fadhaa zetu zote
Fadhaa ni chochote cha huzuni, kusikitisha, kinachochukua amani yako, kinachokufanya usifurahiw maisha na kisichokupa raha nafsini mwako.
Mwambie Mungu fulani (mtaje jina) amekuwa mwiba kwangu.
ongea na Mungu mwambie fadhaa zako zote
Mathayo 11:28
kuna vitu vwili ambavyo vipo hapo
a) Mungu hataki mtu asumbuke yaani unapaswa uishi maisha ya raha, luxurious life
b) Mungu hataki ulemewe. Mwambie hilo linalokulemea kwamba umejaribu peke yako umeshindwa.
Yakobo 5:12 inasema, "Je mtu wa kwenu amepatwa na mabaya? AOMBE. Ana moyo wa kuchangamka na AIMBE ZABURI"
Hii ina maana siku unazokutana na taarifa mbaya au matukio mabaya... BREKI YA KWANZA NI KWA BWANA KUMUELEZA KWA UWAZI NA BILA KIFICHO... UNAVYOJISIKIA... ULIVYOUMIA... KAMA NI KULIA LIA KWELI... KAMA NI KUSHTAKI SHTAKI SANA TU... Lakini hakikisha unatumia TAARIFA MBAYA KAMA MWALIKO WA KUOMBA... Ibilisi hatakuumiza kamwe wala kukuua kama wengine.
Unapoomba, kusali na kushukuru, AMANI YA MUNGU ITAKUFUNIKA NA KUPONYA "MOYO WAKO NA NAFSI YAKO (NIA YAKO)" (Wafilipi 4:6-7).
Na moyo na nafsi zetu kumbe zinaponywa na KUOMBA, KUSALI NA KUMSHUKURU MUNGU badala ya kumlaumu au kulaumu watu au matukio.
Kama tukio limetokea na bado HALIJAKUATHIRI SANA NA KUKUONDOLEA UCHANGAMFU... Huo ni muda mzuri wa KUIMBA ZABURI (Kuanza kumsifu na kumuabudu Mungu)!
Kuna nguvu katika kuabudu na kumsifu Mungu katikati ya jaribu na changamoto.
Paulo na Sila gerezani walisifu na kumuabudu Mungu MILANGO YA GEREZA IKAFUNGUKA KWA UPAKO ULIOSHUKA JUU YAO.
Nakuona ukimsifu na kumuabudu Mungu badala ya kulia na kuomboleza kila hali na taarifa mbaya zijapo na ninamuona Mungu akikuvusha kwenye kila jaribu, pito na gereza katika jina la Yesu!
⚡2 Wakorintho 4:18" tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana, kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele."
chochote kile ambacho kinaonekana au kimeshaokea kwenye mazingira ya nje tayari ni cha muda maadam tu kinaonekana basi ni cha muda tu sio cha kudumu.
Hivyo haijalishi umefanyiwa kitu gani kikaamsha negative hisia ndani yako( uchungu, huzuni, masikitiko, kukosa amani) maadam tu kinaonekana basi ni cha muda tu yaani lazima kitaondoka.
Hapa Biblia inasema tusitazame vinavyoonekana bali tutazame visivyoonekana.
Na visivyo oonekana vinahitaji imani yaani unaangalia vitu jinsi ambavyo neno la Mungu linasema.
πYote yaliyosikiwa au yaliyoonekana haijalishi yamebeba ujumbe gani mbaya kiasi gani hayo ni ya muda tu kwasababu yameshaonekana.
πunapopata zuri lolote kwenye maisha yako ni muda wa weww kutoa muda wako mwingi sana kukiatamia kwenye maombi.
Next levels New devils.
kwa kadiri unavyopata mafanikio na mazuri ndivyo ambavyo na shetani anazidi kukukarbia ili apate nafasi, na mara nyingi sana tunajisahau tunapopata yale tuliyoyategemea.
π ukiona kitu kizuri kimetokea kwenye maisha yako ndio muda wa kuomba kuliko kawaida.
" Udhanipo kuna amani ndipo uharibifu huja"
1 wakorintho 16:9 " kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa wa kufaa sana, na wapo wengi wanipingao"
kwahyo jua kwamba kwenye kila mlango mkubwa uliofunguliwa kwako wapo wengi(hawana idadi) wakupingao.
Ufunuo 12:13-16
Ufunuo 12:4b "na yule joka akasimama mbele za yule mwanamke aliye tayari kuzaaa,ili azaapo amle mtoto wake"
unaona huyu mwanamke anategemea kupata mtoto yaani taarifa njema, lakini yule joka anasubiri azae tu ili amle mtoto wake.
Chochote ambacho unatamani kukizaa kiatamie kwenye maombi ili shetani asikile kwenye elimu yako, kazi yako, ndoa yako, huduma yako, biashara yako nakadhalika.
Ufunuo 12:4 inasema "Ibilisi (joka) alikuwa amesimama mbele ya mwanamke mwenye mimba anayetaka kuzaa ili amle mwanae akimzaa"
Hii ina maana kuna vita kati yako na Ibilisi isiyokoma.
Unapoomba muujiza usifikiri Shetani anakuchekea, anasubiri uje huo muujiza auharibu kabla hujaufaidi!
Angalia "mwanamke anafurahia kuwa anakwenda kuzaa mtoto" asijue Ibilisi yuko hapo karibu anasubiri kuumeza huo muujiza.
Ndio maana watu wanaomba wanapata waume, halafu ndoa (mtoto aliyezaliwa) inakuwa mbovu na inavunjika.
Mtu anaomba kazi, akifika kazini kazi inakuwa uwanja wa vita na anaweza kuamua kuacha (mtoto ameliwa na joka)!
Daka hii:
"Kila muujiza unaotaka kuuzaa Ibilisi anausubiria ili aule"
Ndio maana WATU WANAANZISHA VITU VINAKUFA.
Biashara unaanza vizuri na una uhakika unakwenda kutoka, INALIWA NA JOKA.
Hii ni sababu ya kukufanya UDUMU KUOMBA MPAKA YESU ANARUDI.
HAKUNA BREKI YA MAOMBI RAFIKI YANGU kama unataka vitu vizaliwe!
1Wakorintho 16:9 inasema "Nimefunguliwa mlango mkubwa na wa kufaa sana lakini wako wengi wazuiao/ wanipingao"
Hii ina maana kila ukiona mpenyo, kitu fulani kimetokea, umepata mme, mke, baraka, huduma imekua, umepata mtoto... JIANDAE, KUZIMU NZIMA ITAAMKA KUJARIBU KUUA HUO MLANGO MZURI WA KUFAA.
Ni wajibu wako KUKESHA UKIOMBA ILI MWIZI AJAPO ASIINGIE KWAKO!
UAMUZI NI WAKO.
Unawajibika kuamua ni aina gani ya mawazo uyaruhusu yatawale maisha yako either positively au negatively.
2 Wakorintho 10:3-5
Jinsi ya mwili ni kuangalia vitu vinavyoonekana au taarifa zinasemaje. Yatupasa tuamue kutoka ndani sawasawa na neno lililopo moyoni ili tuwrxe kureact na taarifa mbaya ambazo tunaziona nje
Ni wajibu wako kutiisha kila wazo lako.
Matendo 5:1-11
Waefeso 4:26-27
Yakobo 5:13 -- upatwapo na baya lolote cha kwanza kufanya ***OMBA***
Wafilipi 4:6-7.
cha mwisho pima mawazo yako.
Zaburi 19:14
na ukisoma Wafilipi 4:8 inatufundisha yapi ya kutafakari
1)Yaliyo ya kweli
2)Yaliyo ya staha/ sitirika, bila uchafu
3)Yaliyo ya haki
4)Yaliyo safi
5) Yenye kupendeza
6)Yenye sifa njema
7) Yenye wema wowote
8)Yenye sifa yoyote nzuri
Chochote utakachokitafakari nje ya hzi point nane basi achana nalo lisikuumize kichwa.
Waza na kutafakari aina hizi tu za mawazo.
Mengine nje ya hapo yaangushe na kuyapangua kwa jina la Yesu!
Mwisho kabisa, ni mapenzi ya Mungu tuwe na furaha kila saa ,sekunde, dakika na kila wakati.
Isaya 12:3
"Basi, kwa furaha mtateka maji katika visima vya wokovu"
Mungu anahitaji furaha yako ili umwabudu.
Isaya 55:12
"Maana mtatoka kwa furaha, mtaongozwa kwa amani ....mbele yenu milima na vilima vitatoa nyimbo (hali ngumu zinazozuia wengine kwenu zitakuwa fursa), na miti ya kondeni (wanadamu) itawapigia makofi (watawacelebrate)"
Yohana 16:23-24
"....... hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu iwe timilifu"
Kusudi la Mungu kukujibu maombi yako ni ili ufurahi.
Yesu anawajibika na furaha yako yaani yupo comitted kuhakikisha kila muda unafurahi (Wafilipi 4:4).
Ndiyo maana hakufia dhambi tu msalabani bali pia "HAKIKA AMEYACHUKUA MASIKITIKO YETU, AMEJITWIKA HUZUNI ZETU" (Isaya 53:4).
Kwa hiyo maombi ni opportunity ya kukufanya ufurahi.
Hesabu 23:19
"Mungu si mtu , aseme uongo.....
so ikiwa Mungu amesena na umeona kwenye neno lake lazima atimize"
Nikutakie uanafunzi mzuri.
Urudie na kurudia na kurudia na kisha UYATENDE MOJA BAADA YA JINGINE, mpaka utakapokuwa MASTER WA HISIA ZAKO!
Mwl D.C.K
www.yesunibwana.org
(Tembelea hii website kila mara kukua kiroho)!
Mnenaji: Mwalimu Dickson Cornel Kabigumila.
Tukio: Semina Maalum ya Wadada
Tarehe: 14/02/2016
Utangulizi
⚡Nafsi imegawanyika katika sehem kuu tatu.
1)Hisia (Emotions & Feelings)
2)Maamuzi na machaguo (choices and decisions)
3)Akili (Intellect part)
Na katika somo hili tunajifunza kuhusu hisia.
1)HISIA
Hisia zipo ndani ya mtu tayari na zinaamka zikipata reaction kutoka nje.
Kuna aina mbili za hisia
a) Positive feelings
mfano: furaha, amani, kushangilia nk
b) Negative feelings
mfano: kulia, huzuni, uchungu nk
Vyote hivi vipo ndani ya mtu tayari lakini hadi vipate reaction kutoka nje ndio vitaonekana.
Hisia zinatokana na taarifa kutoka kwenye milango mitano ya ufahamu.
Yaani: Hata Mungu aliyetuumba sisi kwa sura na mfano wake ana hisia hizi za aina mbili:
i)Hasi
Mfano: "Hasira ya Bwana ikawaka"
Au "Mimi ni Mungu mwenye wivu"
Ama
"Wala msimhuzunishe Roho mtakatifu"
Hizi hisia hata Baba yetu anazo lakini anajua namna ya kuzicontrol!
ii) Chanya
"Mungu ni pendo"
Au
"Furaha ya Bwana ni nguvu yetu" ikiwa na maana anafurahi pia.
Lakini anajua namna ya kuzitawala hisia zake.
Hivyo basi, si tatizo kuwa na hisia chanya.
Bali hisia hasi usipojua namna ya kuzitawala na kuzimilki zitakuharibia maisha na watu wengine wanaokuzunguka.
Kumbuka: Hauwezi kuomba ili hasira isiweko kabisa ndani yako, ila unaweza kuomba "hasira isikutawale" (Waefeso 4:26).
Na ni wajibu wako kumnyima nafasi Ibilisi kukulisha taarifa mbaya na kukujeruhi ili kuamsha "hisia hasi" ndani yako ili ufanye dhambi na matukio mabaya!
Jambo jingine la muhimu kujua:
Vichocheo vinavyoamsha hisia hasi (hasira, uchungu, majeraha ya nafsi, visasi) yanakuja kupitia MILANGO MITANO YA FAHAMU.
Unachoona
Unachosikia
Unachogusa/hisi
Unachonusa
Unacholamba
Kama si kizuri, HISIA HASI zitaamka ndani yako na unaweza kufanya mambo ya ajabu.
Jiandae, uko duniani, utaona mengi mabaya ya kuumiza, utasikia taarifa mbaya, utahisi, utagusa na hata kunusa vitu vinavyokera na kuboa.
Mwitikio wako ndio utakaoamua nini utafanya na nini kitajengeka ndani yako.
Ili kushinda hisia mbaya, na majeraha ya nafsi tunapaswa tujue kanuni za Kibiblia za kutawala milango yetu mitano ya fahamu na kila kinachoingia ndani yetu kupitia hiyo!
kwahyo ili tuweze kujicontrol kwenye negative feelings zisituaffect maisha yetu na kuona hatuna sababu yoyote ya kuishi kwasababu ya tarifa uliyosikia au kuona ikaaamsha hisia zako tunapaswa kuwa na taarifa nyingi za neno la Mungu ili ziweze kubadilisha mazingira ya nje.
Hasira, Wivu, huzuni, uchungu vyote hivi vinapaswa viwe controlled na neno la Mungu.
Mungu akusaidie kutembea juu ya kila changamoto kutokana na wingi wa neno lililojaa ndani yako na lenye uvuvio wa Roho Mtakatifu..
❤❤ vitu viwili vinavyokaa karibu na moyo wa mtu
a) Yesu (neno)
Ufunuo 3:20 msaada ambao upo muda wowote.
ukimkataa Shetani then umemkubali Yesu
b) Dhambi
Mwanzo 4:7
ukimkubali shetani then umemkataa Yesu.
Yesu yuko karibu na moyo wako kwa mujibu wa Ufunuo 3:20, akisubiri umpe nafasi akusaidie.
Lakini pia dhambi iko mlangoni kwa moyo wako ikisubiri uliache Neno na agizo la Mungu iingie ndani yako.
Kama ilivyokuwa kwa Kaini (Mwanzo 4:7-8)
Ni wajibu wako kuruhusu nini kiingie na kipi kisiingie MOYONI MWAKO hasa UNAPOPATA TAARIFA MBAYA kutoka kwenye mazingira yako, watu wako, ndugu, mme, mke, watoto, biashara yako nakadhalika.
Ayubu alipopata TAARIFA MBAYA kuhusu wanae, mifugo, mali zake na hata afya yake, HAKUTENDA DHAMBI WALA KUMUWAZIA MUNGU KWA UPUMBAVU (Ayubu 1:22).
Alijua namna ya KUKABILI TAARIFA KUTOKA NJE.
Biblia inasema alichofanya ni "KUMSIFU MUNGU" akisema "JINA LA BWANA LIBARIKIWE"
Ni wajibu wako kujipanga kwa Neno, kwa kumuomba Mungu, na kupata nguvu ya kukabili kila HABARI MBAYA.
"Mwenye haki HATAOGOPA HABARI MBAYA, MOYO WAKE UIMARA UKIMTUMAINI BWANA"
(Zaburi 112:6-7).
Kadri ambavyo UNAKABIDHI MOYO WAKO KWA BWANA... UNA UHAKIKA WA KUTOTETEREKA HABARI MBAYA NA MABAYA YAKITOKEA.
Lakini kadri unavyokuwa unaombea vitu na maisha yako (unavikabidhi kwa Bwana kama Ayubu alivyokuwa akifanya ibada kwa ajili ya wanae na kuwatolea sadaka), unajikuta UNAJUA MUNGU YUKO KAZINI, BILA KUJALI NINI KINAKUTOKEA!
Waebrania 5:7 " Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule,awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu."
hapa tunaona Yesu pia alilia.
wanawake na mabinti wengi huwa tukiumia ni wepesi sana kulia...
Yaan haijalishi umeumizwa kiasi gani usiseme siwezi kuomba nooooo nenda mbele za Mungu kwa machozi na kulia Mungu anasikia aisee.
Stephano pia alilia.
1 Peter 5:7
" huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.
⚡Mungu anajishughulisha sana kwa mambo yetu sio mambo yake ni yetu kwahyo kazi yetu ni kumtika yeye fadhaa zetu zote
Fadhaa ni chochote cha huzuni, kusikitisha, kinachochukua amani yako, kinachokufanya usifurahiw maisha na kisichokupa raha nafsini mwako.
Mwambie Mungu fulani (mtaje jina) amekuwa mwiba kwangu.
ongea na Mungu mwambie fadhaa zako zote
Mathayo 11:28
kuna vitu vwili ambavyo vipo hapo
a) Mungu hataki mtu asumbuke yaani unapaswa uishi maisha ya raha, luxurious life
b) Mungu hataki ulemewe. Mwambie hilo linalokulemea kwamba umejaribu peke yako umeshindwa.
Yakobo 5:12 inasema, "Je mtu wa kwenu amepatwa na mabaya? AOMBE. Ana moyo wa kuchangamka na AIMBE ZABURI"
Hii ina maana siku unazokutana na taarifa mbaya au matukio mabaya... BREKI YA KWANZA NI KWA BWANA KUMUELEZA KWA UWAZI NA BILA KIFICHO... UNAVYOJISIKIA... ULIVYOUMIA... KAMA NI KULIA LIA KWELI... KAMA NI KUSHTAKI SHTAKI SANA TU... Lakini hakikisha unatumia TAARIFA MBAYA KAMA MWALIKO WA KUOMBA... Ibilisi hatakuumiza kamwe wala kukuua kama wengine.
Unapoomba, kusali na kushukuru, AMANI YA MUNGU ITAKUFUNIKA NA KUPONYA "MOYO WAKO NA NAFSI YAKO (NIA YAKO)" (Wafilipi 4:6-7).
Na moyo na nafsi zetu kumbe zinaponywa na KUOMBA, KUSALI NA KUMSHUKURU MUNGU badala ya kumlaumu au kulaumu watu au matukio.
Kama tukio limetokea na bado HALIJAKUATHIRI SANA NA KUKUONDOLEA UCHANGAMFU... Huo ni muda mzuri wa KUIMBA ZABURI (Kuanza kumsifu na kumuabudu Mungu)!
Kuna nguvu katika kuabudu na kumsifu Mungu katikati ya jaribu na changamoto.
Paulo na Sila gerezani walisifu na kumuabudu Mungu MILANGO YA GEREZA IKAFUNGUKA KWA UPAKO ULIOSHUKA JUU YAO.
Nakuona ukimsifu na kumuabudu Mungu badala ya kulia na kuomboleza kila hali na taarifa mbaya zijapo na ninamuona Mungu akikuvusha kwenye kila jaribu, pito na gereza katika jina la Yesu!
⚡2 Wakorintho 4:18" tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana, kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele."
chochote kile ambacho kinaonekana au kimeshaokea kwenye mazingira ya nje tayari ni cha muda maadam tu kinaonekana basi ni cha muda tu sio cha kudumu.
Hivyo haijalishi umefanyiwa kitu gani kikaamsha negative hisia ndani yako( uchungu, huzuni, masikitiko, kukosa amani) maadam tu kinaonekana basi ni cha muda tu yaani lazima kitaondoka.
Hapa Biblia inasema tusitazame vinavyoonekana bali tutazame visivyoonekana.
Na visivyo oonekana vinahitaji imani yaani unaangalia vitu jinsi ambavyo neno la Mungu linasema.
πYote yaliyosikiwa au yaliyoonekana haijalishi yamebeba ujumbe gani mbaya kiasi gani hayo ni ya muda tu kwasababu yameshaonekana.
πunapopata zuri lolote kwenye maisha yako ni muda wa weww kutoa muda wako mwingi sana kukiatamia kwenye maombi.
Next levels New devils.
kwa kadiri unavyopata mafanikio na mazuri ndivyo ambavyo na shetani anazidi kukukarbia ili apate nafasi, na mara nyingi sana tunajisahau tunapopata yale tuliyoyategemea.
π ukiona kitu kizuri kimetokea kwenye maisha yako ndio muda wa kuomba kuliko kawaida.
" Udhanipo kuna amani ndipo uharibifu huja"
1 wakorintho 16:9 " kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa wa kufaa sana, na wapo wengi wanipingao"
kwahyo jua kwamba kwenye kila mlango mkubwa uliofunguliwa kwako wapo wengi(hawana idadi) wakupingao.
Ufunuo 12:13-16
Ufunuo 12:4b "na yule joka akasimama mbele za yule mwanamke aliye tayari kuzaaa,ili azaapo amle mtoto wake"
unaona huyu mwanamke anategemea kupata mtoto yaani taarifa njema, lakini yule joka anasubiri azae tu ili amle mtoto wake.
Chochote ambacho unatamani kukizaa kiatamie kwenye maombi ili shetani asikile kwenye elimu yako, kazi yako, ndoa yako, huduma yako, biashara yako nakadhalika.
Ufunuo 12:4 inasema "Ibilisi (joka) alikuwa amesimama mbele ya mwanamke mwenye mimba anayetaka kuzaa ili amle mwanae akimzaa"
Hii ina maana kuna vita kati yako na Ibilisi isiyokoma.
Unapoomba muujiza usifikiri Shetani anakuchekea, anasubiri uje huo muujiza auharibu kabla hujaufaidi!
Angalia "mwanamke anafurahia kuwa anakwenda kuzaa mtoto" asijue Ibilisi yuko hapo karibu anasubiri kuumeza huo muujiza.
Ndio maana watu wanaomba wanapata waume, halafu ndoa (mtoto aliyezaliwa) inakuwa mbovu na inavunjika.
Mtu anaomba kazi, akifika kazini kazi inakuwa uwanja wa vita na anaweza kuamua kuacha (mtoto ameliwa na joka)!
Daka hii:
"Kila muujiza unaotaka kuuzaa Ibilisi anausubiria ili aule"
Ndio maana WATU WANAANZISHA VITU VINAKUFA.
Biashara unaanza vizuri na una uhakika unakwenda kutoka, INALIWA NA JOKA.
Hii ni sababu ya kukufanya UDUMU KUOMBA MPAKA YESU ANARUDI.
HAKUNA BREKI YA MAOMBI RAFIKI YANGU kama unataka vitu vizaliwe!
1Wakorintho 16:9 inasema "Nimefunguliwa mlango mkubwa na wa kufaa sana lakini wako wengi wazuiao/ wanipingao"
Hii ina maana kila ukiona mpenyo, kitu fulani kimetokea, umepata mme, mke, baraka, huduma imekua, umepata mtoto... JIANDAE, KUZIMU NZIMA ITAAMKA KUJARIBU KUUA HUO MLANGO MZURI WA KUFAA.
Ni wajibu wako KUKESHA UKIOMBA ILI MWIZI AJAPO ASIINGIE KWAKO!
UAMUZI NI WAKO.
Unawajibika kuamua ni aina gani ya mawazo uyaruhusu yatawale maisha yako either positively au negatively.
2 Wakorintho 10:3-5
Jinsi ya mwili ni kuangalia vitu vinavyoonekana au taarifa zinasemaje. Yatupasa tuamue kutoka ndani sawasawa na neno lililopo moyoni ili tuwrxe kureact na taarifa mbaya ambazo tunaziona nje
Ni wajibu wako kutiisha kila wazo lako.
Matendo 5:1-11
Waefeso 4:26-27
Yakobo 5:13 -- upatwapo na baya lolote cha kwanza kufanya ***OMBA***
Wafilipi 4:6-7.
cha mwisho pima mawazo yako.
Zaburi 19:14
na ukisoma Wafilipi 4:8 inatufundisha yapi ya kutafakari
1)Yaliyo ya kweli
2)Yaliyo ya staha/ sitirika, bila uchafu
3)Yaliyo ya haki
4)Yaliyo safi
5) Yenye kupendeza
6)Yenye sifa njema
7) Yenye wema wowote
8)Yenye sifa yoyote nzuri
Chochote utakachokitafakari nje ya hzi point nane basi achana nalo lisikuumize kichwa.
Waza na kutafakari aina hizi tu za mawazo.
Mengine nje ya hapo yaangushe na kuyapangua kwa jina la Yesu!
Mwisho kabisa, ni mapenzi ya Mungu tuwe na furaha kila saa ,sekunde, dakika na kila wakati.
Isaya 12:3
"Basi, kwa furaha mtateka maji katika visima vya wokovu"
Mungu anahitaji furaha yako ili umwabudu.
Isaya 55:12
"Maana mtatoka kwa furaha, mtaongozwa kwa amani ....mbele yenu milima na vilima vitatoa nyimbo (hali ngumu zinazozuia wengine kwenu zitakuwa fursa), na miti ya kondeni (wanadamu) itawapigia makofi (watawacelebrate)"
Yohana 16:23-24
"....... hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu iwe timilifu"
Kusudi la Mungu kukujibu maombi yako ni ili ufurahi.
Yesu anawajibika na furaha yako yaani yupo comitted kuhakikisha kila muda unafurahi (Wafilipi 4:4).
Ndiyo maana hakufia dhambi tu msalabani bali pia "HAKIKA AMEYACHUKUA MASIKITIKO YETU, AMEJITWIKA HUZUNI ZETU" (Isaya 53:4).
Kwa hiyo maombi ni opportunity ya kukufanya ufurahi.
Hesabu 23:19
"Mungu si mtu , aseme uongo.....
so ikiwa Mungu amesena na umeona kwenye neno lake lazima atimize"
Nikutakie uanafunzi mzuri.
Urudie na kurudia na kurudia na kisha UYATENDE MOJA BAADA YA JINGINE, mpaka utakapokuwa MASTER WA HISIA ZAKO!
Mwl D.C.K
www.yesunibwana.org
(Tembelea hii website kila mara kukua kiroho)!
Subscribe to:
Posts (Atom)